Utaratibu wa Vipengele vya Kirai Nomino katika Kiswahili

  • Chege Joel Ngari Chuo Kikuu Cha Kenyatta
  • Leonard Chacha Mwita, PhD Chuo Kikuu Cha Kenyatta
Keywords: Eksibaa, Muundo, Kirai
Sambaza Makala:

Ikisiri

Lugha zote ulimwenguni huwa na sheria zake zinazohusu mfuatano wa maneno katika sentensi. Hivyo basi, kama zilivyo lugha zingine, lugha ya Kiswahili vilevile ina utaratibu mwafaka ambao vivumishi katika kirai nomino (KN) hufuata ili kuibua sentensi kubalifu sio kimantiki tu, bali pia kisarufi, jambo ambalo huathiri maana ya KN husika. Makala haya yameweka bayana utaratibu wa vipengele vya kirai nomino katika Kiswahili. Nadharia ya Eksibaa iliyoasisiwa na Noam Chomsky ilitumika. Nadharia ya Eksibaa ni nadharia ya muundo virai inayoonyesha kategoria za sintaksia zinazofungamanishwa na nomino. Mbinu za utafiti zilizoongoza utafiti huu ni hojaji na mahojiano. Mbinu ya uchunzaji ilitumika ambapo maongezi ya wazungumzaji yalirekodiwa. Mbinu husika zilikamilishana na kujengana kila mojawazo ikifidia mapungufu ya nyingine. Sampuli ya utafiti huu iliteuliwa kwa kutumia mbinu kusudio. Utafiti huu ulishirikisha watafitiwa 120 ili kuafiki lengo husika. Walengwa wa utafiti huu walikuwa ni: wahadhiri na walimu, vijana waliomaliza shule ya upili na vyuo na wanafunzi wa shule za upili na vyuo. Matokeo ya utafiti huu yalidhihirisha makundi matatu ya utaratibu wa vipengele vya kirai nomino ambayo ni: kirai nomino cha kiwakilishi na vivumishi, kirai nomino chenye nomino vivumishi na kishazi tegemezi na mwisho ni kirai nomino cha nomino, kitenzi jina na kivumishi. Matokeo ya utafiti huu yatapanua uelewa wa kirai nomino kwa mitazamo tofauti na hivyo kuongeza maarifa kuhusiana na dhana husika. Vilevile, mapendekezo ya utafiti huu yatakuwa ya manufaa kwa wanafunzi, waandishi wa vitabu, Wizara ya Elimu, serikali, wapangaji mitaala, watafiti wa baadaye na walimu chipukizi kupanua ufahamu na uelewa wa tawi la isimu ambalo ni pragmatiki.

Upakuaji

Bado hatuna takwimu za upakuaji.

Marejeleo

Chomsky, N. (1970). Remarks on Nominalization. In: R. Jacobs and P. Rosenbaum (eds.), Readings in English Transformational Grammar, Ginn, Waltham, MA, 184-221.

Chomsky, N. (1981). Lectures on Government and Binding. Bordrecht: Foris Publication.

Haegeman, L (1994). Introduction to Government & Binding Theory, 2nd ed. Oxford: Blackwell.

Haegeman, L. (1991). Introduction to Government and Binding Theory: U.K, Blackwell Publishers.

Kothari, C.R. (2009). Research Methodology. Methods and Techniques (Toleo la pili), New Delhi; New Age International (P) Limited Publishers.

Masebo, J. na Nyangwine. (2007). Nadharia ya Lugha Kiswahili 1 Kidato cha 5&6, Dar-es-Salaam: Nyambari Nyangwine Publishers.

Massamba na wenzake. (2009). Kamusi ya Isimu na Falsafa ya Lugha. TUKI, Chuo Kikuu cha Dar-es-Salaam. TUKI.

Matinde. S. (2012). Dafina ya Lugha. Isimu na Nadharia. Dar es Salaam: Serengeti Educational Publishers.

Oxford, R. (2011). Kiswahili Kidato cha 5-6. Dar es Salaam: Oxford University Press Tanzania Ltd.

Radford, A. (2004). English Syntax: An Introduction. Great Britain: Cambridge University Press.

Vincent, S. (2010). The Constituent Structure of the Swahili Noun Phrase. Tasnifu ya uzamili (haijachapishwa): Chuo Kikuu cha Dar es Salaam.

Tarehe ya Uchapishaji
29 September, 2022
Jinsi ya Kunukuu
Ngari, C., & Mwita, L. (2022). Utaratibu wa Vipengele vya Kirai Nomino katika Kiswahili. Jarida La Afrika Mashariki La Masomo Ya Kiswahili, 5(1), 297-313. https://doi.org/10.37284/jammk.5.1.826

Makala zilizo somwa zaidi kama hii.