Athari za Usasa kwenye Usimulizi wa Hadithi katika Jamii ya Wamasaaba Nchini Uganda

  • Willy Wanyenya, PhD Makerere University Business School
  • Rocha Chimerah, PhD Pwani University
  • Nancy Jumwa Ngowa Pwani University
Keywords: Usasa, Hadithi, Sanaa, Fasihi
Sambaza Makala:

Ikisiri

Katika makala haya, watafiti anaeleza jinsi usimulizi wa hadithi umeathiriwa na usasa katika jamii ya Wamasaaba nchini Uganda. Anafanya hivyo kwa kulinganisha hali ilivyo sasa na jinsi ilivyokuwa kabla Wazungu hawajazuru barani Afrika. Mtafiti analinganisha miktadha ya utendaji wa hadithi na anatoa maelezo kuhusu mitindo mbalimbali ya utendaji. Anaeleza jinsi Waafrika walivyosimulia watoto wao hadithi kabla ya Wazungu kuja barani humu. Kwenye kazi hii, madhumuni ya utafiti ni: kudhihirisha athari za usasa kwenye masimulizi ya kinathari. Pili, kueleza stadi zilizokuwa zikitumiwa na Waafrika katika usimulizi wa hadithi. Mkabala wa utafiti ulikuwa wa nyanjani. Kwa kutumia mkabala huu, mtafiti alizuru nyanjani halafu akaanza kuendeleza mahojiano na wahojiwa wake. Kabla hajafanya hivyo, mtafiti alijitambulisha kwa wahojiwa wake na kuwaambia sababu za utafiti wake. Alifanya hivyo ili kuwaondolea wasiwasi. Majibu ya wahojiwa yalijumlisha data ambazo zilihitajika na mtafiti. Matokeo ya utafiti yanaonyesha kuwa usimulizi wa hadithi umefifia sana katika jamii ya Wamasaaba kutokana na usasa. Sababu ambazo zimepelekea usimulizi wa hadithi kufifia jamii hii pia zimeelezwa. Miongoni mwa sababu hizo ni: ulevi ambao hufanya watu kurejea nyumbani wakiwa wamelewa na kushindwa kusimulia watoto wao hadithi. Sababu nyingine ni wazazi kuthamini elimu ya kisasa na kuacha utamaduni wao wa kulea watoto ili baadaye wawe wake na waume wazuri. Wazazi kuhamasisha watoto wao wasome vitabu badala ya kuwasimulia hadithi. Nne, wazazi kuwa na lengo la kuelimisha watoto wao ili baadaye wapate kazi za afisi. Tano, jambo la kuwepo na utandawazi ambalo limepelekea watu kujumuika na kuiga tamaduni za kigeni. Upeo wa utafiti huu ulihusika na mabadiliko kwenye usimulizi wa hadithi na sababu ambazo zimepelekea utamaduni wa kusimulia hadithi kufifia katika jamii ya Wamasaaba nchini Uganda. Mtafiti alitumia mbinu ya bahati nasibu kuteua sampuli za wahojiwa.

Upakuaji

Bado hatuna takwimu za upakuaji.

Marejeleo

Crăciun, D., Crăciun, P., & Bunoiu, M. (2016, March). Digital storytelling as a creative teaching method in Romanian science education. In AIP Conference Proceedings (Vol. 1722, No. 1, p. 310001). AIP Publishing LLC.

Cueva, M., Kuhnley, R., Revels, L., Schoenberg, N. E., & Dignan, M. (2015). Digital storytelling: a tool for health promotion and cancer awareness in rural Alaskan communities. International Journal of Circumpolar Health, 74(1), 28781.

Fikriah, F. (2016). Using the Storytelling Technique to Improve English Speaking Skills of Primary School Students. English Education Journal, 7(1), 87-101.

Foley, L. M. (2013). Digital storytelling in primary-grade classrooms. PhD Thesis. Arizona State University.

Juppi, P. (2015). Using Digital Storytelling to Enhance Digital Participation–A Case Study from Tanzania. Arts Academy, Turku University Press, Turkuamkfi, Turkey.

Kervin, L., McMahon, S., O'Shea, S. E., & Harwood, V. (2014). Digital storytelling: Capturing the stories of mentors in Australian Indigenous Mentoring Experience. University of Wollongong.

Meadows, D. (2003). Digital Storytelling: Research-Based Practice in New Media. Visual Communication, 2, 189-193.

Mooney, A., & Prins, E. (2015). Digital Storytelling in Family Literacy Programs. Practitioner's Guide# 5. Goodling Institute for Research in Family Literacy, Penn State College of Education.

Ndalichako, J. (2017). Fasihi Simulizi na Sayansi na Teknolojia. Dar es Salaam, TZ: Taasisi ya Uchunguzi wa Taaluma za Kiswahili, Chuo Kikuu cha Dar es Salaam.

Porter, B. (2005). The art of digital storytelling. Part I: Becoming 21st Century Story Keepers. Revista Discovery Education

Robin, B. R. (2016). The power of digital storytelling to support teaching and learning. Digital Education Review, (30), 17-29.

Smeda, N., Dakich, E., & Sharda, N. (2014). The effectiveness of digital storytelling in the classrooms: a comprehensive study. Smart Learning Environments, 1(1), 6.

Yamac, A., & Ulusoy, M. (2017). The effect of digital storytelling in improving the third graders' writing skills. International Electronic Journal of Elementary Education, 9(1), 59-86.

Tarehe ya Uchapishaji
8 September, 2020
Jinsi ya Kunukuu
Wanyenya, W., Chimerah, R., & Ngowa, N. (2020). Athari za Usasa kwenye Usimulizi wa Hadithi katika Jamii ya Wamasaaba Nchini Uganda. Jarida La Afrika Mashariki La Masomo Ya Kiswahili, 2(2), 116-127. https://doi.org/10.37284/eajss.2.2.206

Makala zilizo somwa zaidi kama hii.