Visababishi vya Idadi Kubwa ya Wanafunzi wa Shule za Sekondari Nchini Uganda Kutochukua Somo la Kiswahili

  • Willy Wanyenya, PhD Makerere University Business School
Sambaza Makala:

Ikisiri

Katika makala haya, mtafiti anaeleza visababishi vya idadi kubwa ya wanafunzi katika shule za upili nchini Uganda kutochukua somo la Kiswahili. Wakati wa kupunguza idadi ya masomo kwa kila mwanafunzi unapofika, wanafunzi huwa na sababu za kimsingi zinazowafanya wapendelee masomo fulani na kuyakataa mengine. Kwa kawaida wanafunzi huwa hawalazimishwi kuchukua masomo fulani. Kila mwanafunzi huwa na uhuru wa kuchagua masomo anayoyapenda. Imebainika wazi kuwa nchini Uganda, wakati wa wanafunzi kupunguza idadi ya masomo unapofika, wengi wao huwa wanaacha somo la Kiswahili. Katika darasa la wanafunzi mia moja, ni wanafunzi kumi au kumi na watano tu ndio wanachukua Kiswahili. Hali hii inatisha sana hasa kwa wapenzi wa Kiswahili. Hivyo basi, mtafiti aliendeleza utafiti huu ili kueleza sababu zinazopelekea wanafunzi kufanya hivyo. Dhamira ya utafiti ni kueleza bayana kwa nini wanafunzi wengi nchini Uganda huwa hawachukui somo la Kiswahili. Madhumuni ya utafiti huu ni kueleza mielekeo ya wanafunzi wa shule za sekondari nchini Uganda dhidi ya ujifunzaji wa lugha ya Kiswahili na kufafanua hatua ambazo zinastahili kuchukuliwa ili kufanya idadi ya wanafunzi wa Kiswahili iongezeke. Katika kazi hii, mkabala wa utafiti ulikuwa wa nyanjani. Kwa kutumia mkabala huu, mtafiti alizuru nyanjani na kuendeleza mahojiano na wahojiwa wake. Utafiti huu umeonyesha kuwa wanafunzi wa shule za sekondari nchini Uganda huwa hawapendelei somo la Kiswahili kwa sababu zifuatazo: kuwepo na sera mbovu nchini kuhusu lugha ya Kiswahili; wanafunzi kutokuwa na msingi wa lugha ya Kiswahili; wanafunzi kuwa na fikra potovu kuwa Kiswahili ni lugha ya wezi; wanafunzi kufikiria kuwa Kiswahili ni somo linalofaa wenzao kutoka Kenya na Tanzania; wanafunzi kufikiria kuwa lugha ya Kiswahili ni ngumu; watu wa nchi ya Uganda kuchukulia Kiswahili kuwa lugha ya kawaida na isiyofaa kufundishwa shuleni; wananchi wa Uganda kupendelea Kiganda na Kiingereza na kupiga vita lugha ya Kiswahili.

Upakuaji

Bado hatuna takwimu za upakuaji.

Marejeleo

Abdelkader, M., & Amine, D. M. (2017). Exploring students’ attitudes towards learning English as a foreign language A semi-structured research interviewing with third year LMD students at Saida University. Aleph, 8, 89-109.

Abidin, M, Mohammadi, M. & Alzwari, H. (2012). EFL Students’ Attitudes towards Learning English Language: The Case of Libyan Secondary School Students. Asian Social Science, 8(2), 119-134.

Abu-Snoubar, T. K. (2017). An Evaluation of EFL Students’ Attitudes Toward English Language Learning in Terms of Several Variables. International Journal of English Language Teaching, 5(6), 18-34.

Ahmed, S. (2015). Attitudes towards English Language Learning among EFL Learners at UMSKAL. Journal of education and practice, 6(18), 6-16.

Al Noursi, O. (2013). Attitude towards Learning English: The case of the UAE Technological High School. Educational Research, 4(1), 21-30.

Al-Musnad, B. I. (2018). The Role of Motivation and Attitude in Second Language Learning: A study of Arabic Language Learning among Foreign Female Nurses in Riyadh, Saudi Arabia. Journal of Applied Linguistics and Language Research, 5(1), 157-183.

Choy, S., & Troudi, S. (2006). An investigation into the changes in perceptions of and attitudes towards learning English in a Malaysian college. International Journal of Teaching and Learning in Higher Education, 18(2), 120-130.

Eshghinejad, S. (2016). EFL Students’ Attitudes toward Learning English Language: The Case Study of Kashan University Students. Cogent Education, 3(1), 1-13.

Fatiha, M., Sliman, B., Mustapha, B., & Yahia, M. (2014). Attitudes and motivations in learning English as a foreign language. International Journal of Arts & Sciences, 7(03), 117-128.

Habók, A., & Magyar, A. (2018). The effect of language learning strategies on proficiency, attitudes and school achievement. Frontiers in psychology, 8, 2358.

Horwitz, E. K. (1987). Surveying student beliefs about language learning. In A. Wenden, & J. Rubin (Eds.), Learner strategies in language learning (pp. 119-129). Englewood Cliffs, NJ: Prentice-Hall.

Hosseini, S. B., & Pourmandnia, D. (2013). Language learners’ attitudes and beliefs: Brief review of the related literature and frameworks. International Journal on New Trends in Education and Their Implications, 4(4), 63-74.

Karahan, F. (2007). Language attitudes of Turkish students towards the English language and its use in Turkish context. Cankaya University Journal of Arts and Sciences, 1(7), 73-87.

Kovac, M. M., & Zdilar, A. M. (2017). Students’ attitudes towards foreign languages. Journal of Education and Developmental Psychology, 7(2), 124-133.

Latchanna, G., & Dagnew, A. (2009). Attitude of teachers towards the use of active learning methods. E-journal of All India Association for Educational Research, 21(1).

Mingyong, Z. (2015, February). The effect of attitude on foreign language learning and teaching in institutes of higher vocational education based on affective filter hypothesis. In 2015 International Conference on Futuristic Trends on Computational Analysis and Knowledge Management (ABLAZE) (pp. 728-733). IEEE.

Nilay, A. V. C. I. (2018). Attitudes of state school students towards learning English as a foreign language. Uluslararası Güncel Eğitim Araştırmaları Dergisi, 4(1), 41-51.

Oroujlou, N., & Vahedi, M. (2011). Motivation, attitude, and language learning. Procedia-Social and Behavioral Sciences, 29, 994-1000.

Rahimi, M., & Yadollahi, S. (2011). Foreign language learning attitude as a predictor of attitudes towards computer-assisted language learning. Procedia Computer Science, 3, 167-174.

Smith, A. N. (1971). The importance of attitude in foreign language learning. The Modern Language Journal, 55(2), 82-88.

Victori, M., & Lockhart, W. (1995). Enhancing metacognition in self-directed language learning. System, 23, 223-234

Tarehe ya Uchapishaji
5 June, 2020
Jinsi ya Kunukuu
Wanyenya, W. (2020). Visababishi vya Idadi Kubwa ya Wanafunzi wa Shule za Sekondari Nchini Uganda Kutochukua Somo la Kiswahili. Jarida La Afrika Mashariki La Masomo Ya Kiswahili, 2(2), 1-10. https://doi.org/10.37284/eajss.2.2.159

Makala zilizo somwa zaidi kama hii.