Vipengele vya Mwingilianomatini katika Ujenzi wa Maudhui ya Umaskini: Mfano Katika Musaleo! na Bina-Adamu!
Ikisiri
Makala haya yanatathmini matumizi ya vipengele vya mwingilianomatini (MM) katika ujenzi na uwasilishaji wa maudhui ya kazi za Kiswahili. Uchanganuzi huu ni wa kimaktaba kufuatia mihimili ya nadharia ya Mwingilianomatini. Riwaya za Musaleo! na Bina-Adamu zilichaguliwa kimakusudi kwa sababu mwingilianomatini umetumiwa kujenga dhamira ya umaskini. Maudhui ya ulitima katika riwaya za Musaleo! na Bina-Adamu yamechaguliwa ili kudhihirisha jinsi suala sumbufu ulimwenguni linaweza kuwasilishwa kwa njia mbalimbali. Waandishi wa kisasa wa fasihi wamechangamkia mno matumizi ya mbinu ya mwingilianomatini katika ujenzi wa dhamira za kazi zao. Riwaya za Musaleo! na Bina-Adamu za Wamitila zilirejelewa kama mifano ya kazi zilizojengwa Ki-MM. Riwaya za kisasa ni muhimu katika jamii kwani maandishi yanahusu masuala yanayomkumba binadamu katika ulimwengu wake sasa, anapojaribu kujitambua na kujieleza.
Upakuaji
Copyright (c) 2019 Esther J Korir, Issa Mwamzandi, PhD, Simiyu` Kisurulia, PhD
This work is licensed under a Creative Commons Attribution 4.0 International License.