Maudhui katika Nyimbo Teule Kwenye Kipindi cha Rauka

  • Joyce Chepkwony Catholic University of Eastern Africa
  • Fred Wanjala Simiyu, PhD Kibabii University
  • Margan Adero Catholic University of Eastern Africa
Sambaza Makala:

Ikisiri

Utafiti huu unahusu maudhui katika nyimbo teule kwenye vyombo vya habari, mfano ni nyimbo katika kipindi cha Rauka katika runinga ya Citizen. Utafiti ulichochewa na haja ya kutaka kuchunguza nafasi ya vyombo vya habari katika kuhuisha fasihi simulizi kupitia utanzu wa nyimbo. Tafiti za awali zilichunguza tanzu nyingine kama mazungumzo na maigizo. Utafiti huu ulidhamiria hususan: Kubainisha vigezo vilivyotumiwa kuteua nyimbo zinazochezwa kwenye kipindi cha Rauka; Kuonyesha maudhui katika nyimbo teule; Kuchunguza mbinu za lugha zilizotumiwa kuwasilisha maudhui za nyimbo zinazoteuliwa na kuchezwa kwenye kipindi cha Rauka. Utafiti huu ulifanywa kwa kuzingatia muundo wa kimfano unaoeleza kuwa mtafiti huteua eneo au kitu maalum ambacho kitashughulikiwa na kuwezesha kupatikana kwa data za utafiti zilizokusudiwa.  Utafiti huu uliongozwa na nadharia ya Ajenda iliyoasisiwa na McCombs na Shaw mwaka wa 1972. Nadharia ya Ajenda ilitumika kuhakiki uteuzi wa nyimbo wa kipindi kinachopeperushwa na runinga. Uchunguzi ulifanywa katika idhaa ya Citizen kipindi cha Rauka kinachopeperusha nyimbo za dini. Utafiti uliwahusisha waandaaji wawili wa kipindi cha Rauka cha runinga ya Citizen na watazamaji 68 kutoka eneo la Eldoret, Kaunti ya Uasin Gishu, shule za upili ya wasichana ya Hill School. Kwa ujumla, utafiti uliwahusisha watu 70. Watazamaji waliteuliwa kwa kutumia usampulishaji kimaksudi. Vifaa vifuatavyo vilitumiwa kukusanya data: hojaji kwa watazamaji, usaili kwa waandaaji wa kipindi na mwalimu msimamizi wa masuala ya dini na mkuu wa ushauri na nasaha na kinasa sauti kunasia vipindi vilivyoteuliwa kisha vikachanganuliwa. Data ifuatayo ilikusanywa: Nyimbo zilizochezwa kwenye kipindi cha Rauka ziliteuliwa kwa kuzingatia mada ya siku, muda uliotengewa kipindi cha Rauka, hadhira, masuala ibuka, kuwepo na nyimbo zinazowavutia watazamaji; Utafiti umebainisha kuwa nyimbo zinazochezwa katika kipindi cha Rauka zina maudhui ya upendo, shukrani, msamaha, uvumilivu, heshima, wema na msaada. Data iliyokusanywa ilichanganuliwa kwa kuzingatia nadharia ya Ajenda kwa kubainisha maudhui yaliyomo kisha matokeo yakawasilishwa kupitia maelezo ya kifafanuzi na mfano. Matokeo ya utafiti huu yatakuwa mchango kwa tafiti ambazo zimefanywa kuhusu fasihi simulizi na matumizi yake katika vyombo vya habari. Utafiti huu vilevile utakuwa wa manufaa kwa yeyote atakayefanya utafiti kuhusu fasihi simulizi na vyombo vya habari.

Upakuaji

Bado hatuna takwimu za upakuaji.

Marejeleo

Behr, R. L., & Iyengar, S. (1985). Television news, real-world cues, and changes in the public agenda. Public Opinion Quarterly, 49(1), 38-57.

Beja, S. K. (2000). Giriama funeral songs: a functional aesthetic study (Doctoral dissertation, University of Nairobi).

Carey, J. R., Clicque, S. H., Leighton, B. A., & Milton, F. (1976). A test of positive reinforcement of customers. Journal of Marketing, 40(4), 98-100.

Collins, H. (1979). Collins English Dictionary. Great Britain: Harper Collins Publishers

MacFarland, D. (1990). Contemporary radio programming strategies. Hillsdale, NJ: Lawrence Erlbaom Associates.

Matteru, M. (1981). Fasihi simulizi na uandishi makala ya semina ya waandishi wa Kiswahili: Dar es salaam.

McCombs, M. E., & Shaw, D. L. (1972). The agenda-setting function of mass media. Public opinion quarterly, 36(2), 176-187.

Senkoro, F. (1979). Fasihi; Press and Publicity Centre. Dar es salaam.

Wamitila, K. (2003). Kichocheo cha Fasihi: Simulizi na Andishi: Focus Publications Ltd.

Wamitila, K. (2008). Kanzi ya Fasihi Misingi ya Uchanganuzi wa Fasihi. Nairobi: Vide~muwa Publishers Ltd.

Wanjala, F. (2013). Kitovu cha Fasihi Simulizi kwa Shule. Vyuo na Ndaki. Mwanza: Serengeti Educational Publishers(T) LTD.

Wanta, W. (1988). The effects of dominant photographs: An agenda-setting experiment. Journalism Quarterly, 65(1), 107-111.

Wasike, D. (2017). Lugha kama rasilimali ya jamii: Uchunguzi wa redio za FM zinazotumia kibukusu katika kaunti ya Bungoma. Tasnifu ya uzamifu chuo kikuu cha Moi.

Wasike, M. D. (2017). Lugha kama rasilimali ya jamii: uchunguzi wa redio za fm zinazotumia kibukusu katika kaunti ya bungoma (Doctoral dissertation, Moi University).

Tarehe ya Uchapishaji
15 July, 2020
Jinsi ya Kunukuu
Chepkwony, J., Simiyu, F., & Adero, M. (2020). Maudhui katika Nyimbo Teule Kwenye Kipindi cha Rauka. Jarida La Afrika Mashariki La Masomo Ya Kiswahili, 2(2), 32-43. https://doi.org/10.37284/eajss.2.2.183

Makala zilizo somwa zaidi kama hii.