Darasa za Kimaharajani za Nyakanga-Kungwi-Sheikh Juma Amiri Kuhusu Unyumba
Ikisiri
Lugha ya kimaharajani iliangaziwa mwanzo na Mikhail Bakhtin, mwanaisimu wa Kirusi na mwitifaki mkuu wa Usemezano. Lugha hii ina sifa za kuweka kanro kaida za usemaji wa kirasmi na kuwacha wananchi watangamane bila vizuizi vya kiutawala. Hudhihirisha bezo, ucheshi, upuzi kwa uwazi na kila mshiriki akafurahiya hali hii. Kulingana na Bakhtin niya haswa ni kupata hisiya za nrani za watawaliwa, lakini kwa kauli nyengine, watawala huzitumiya fununu hizi kuzidi kuwatawala wananchi; hichi ndicho kinaya cha umaharajani. Katika lugha na fasihi ya Kiswahili dhana ya umaharajani bado haijashughulikiwa ipasavyo seuze maswala ya kidini. Sheikh Juma Amiri ameweza kupata umaarufu na kuenreleya kualikwa katika hafla mbalimbali Kenya na Afrika Mashariki kwa sababu ya kuelezeya maswala ya unyumba kwa uwazi unaoonesha kukiuka kaida za shekhe wa Kiislamu. Makala haya yameonesha namna Sheikh Juma Amiri anavotumiya maneno, matenro, uigo, sauti, na ishara za mwili kuelezeya mambo ya unyumba namna yalivozorota, yanavozorotesha jumuiya ya Waislamu na anapendekeza mbinu mpya wananrowa wazitumiye ili wafaulishe nrowa zao. Anasuta wanaume, wanawake, mashekhe, wazazi kwa maneno yaliyojaa jazanra na piya hutumiya maneno yatakayochukuliwa ni kufuru lau si umaharajani. Anapomaliza darasa zake hadhira inachanganyikiwa kutojuwa Sheikh Juma Amiri ni nyakanga, kungwi, au ni shekhe? Makala haya yanahitimisha kuwa kwa kutumiya mbinu hii ya kimaharajani, Sheikh Juma Amiri amefaulu kufikisha ujumbe wake kiucheshi na kuwateka kimawazo walengwa watake kumsikiza kila mahali kila wakati.
Upakuaji
Copyright (c) 2019 Mohamed Karama, PhD
This work is licensed under a Creative Commons Attribution 4.0 International License.