Vikwazo vya Usimilishaji wa Ishara za Isimu katika Breili

  • Daniel Mburu Mwangi, PhD Chuo Kikuu cha Kenyatta
Keywords: Vikwazo Vya Usimilishaji, Breili, Isimu, Ishara Za Breili
Sambaza Makala:

Ikisiri

Utafiti huu ulinuia kuchanganua usimilishaji wa ishara za isimu katika breili ya Kiswahili. Uchanganuzi huu ulitiwa hamasa na mambo matano muhimu. Kwanza, breili ndio njia ya pekee ya uandishi ambayo watu wasioona hutumia katika mawasiliano na usomi wao. Vilevile, kutokuwepo kwa kipengele muhimu cha matamshi katika kamusi za breili na vitabu vya sarufi hasa vya sekondari. Jambo jingine ni kwamba, wanafunzi wanaotumia breili hupewa maswali mbadala wakati wanapotahiniwa katika maeneo ya fonolojia, mofolojia, na hata katika uchanganuzi wa sentensi. Aidha, kutokuwepo kwa ishara bainifu za isimu katika maandishi ya breili ya Kiswahili. Kichocheo cha mwisho, praima mbili za breili ya Kiswahili: ya 1978 na 1995 zinazotumiwa Afrika Mashariki hazina ishara za kiisimu. Utafiti huu ulikusudia kujibu maswali yafuatayo: changamoto zipi zinazozuia usimilishaji wa ishara za kiisimu katika breili ya Kiswahili? Rasimu za Kiingereza na Kiswahili huathiriana kwa njia zipi? Ukosefu wa ishara za isimu katika breili huathiri ufundishaji wa isimu kwa njia gani?  Na mwisho, mikato ya Kiswahili na ya Kiingereza inayotumia nukta zinazofanana huathiri uchapishaji wa vitabu vya isimu kwa njia zipi? Utafiti huu ulilenga kutimiza malengo yafuatayo – kwanza, kubainisha na kutatua changamoto zinazozuia usimilishaji wa ishara za isimu katika breili ya Kiswahili. Pili, Kuchanganua rasimu ya Kiingereza na ya Kiswahili. Aidha, kuchunguza athari ya ukosefu wa ishara hizi katika ufundishaji wa isimu. Mwisho, kutathmini athari ya matumizi ya mikato inayotumia nukta zinazofanana katika uchapishaji wa vitabu vya isimu. Makala haya yameshughulikia vikwazo vya usimilishaji wa ishara za isimu katika breili. Mtafiti alitumia mbinu ya mahojiano katika kukusanya dataUtafiti huu ulichanganua usimilishaji wa ishara hizi kwa kuzingatia nadharia ya usomaji na uandishi wa breili iliyoasisiwa na Kizuka na Fuji (2005). Mtafiti aligundua kuwa uchache wa nukta nundu umesababisha uradidi mwingi wa matumizi ya nukta nundu hizi. Uradidi huu umechangia kuwepo kwa utata  wa kimaana katika fonolojia na sintaksia ya Kiswahili, vikwazo vya ufundishaji wa isimu miongoni mwa wanafunzi wasioona, makosa katika vitabu vya sarufi hasa kidato cha kwanza na kidato cha pili na changamoto zinazotinga usimilishaji wa ishara za kiisimu katika Breili. Utafiti huu utawafaidi wanafunzi wanaotumia breili na walimu na wahadhiri wanaofunza isimu

Upakuaji

Bado hatuna takwimu za upakuaji.

Marejeleo

Ipara, I., & Maina, G. (2013). Fani ya Isimujamii kwa shule za sekondari. Oxford University Press.

Prima (1978). Kiswahili Braille: KIB.

Prima (1993). Kiswahili Braille: KIB.

Kiango, J. G. (2002). Nafasi ya Kiswahili katika ujenzi wa jamii mpya ya Afrika Mashariki. Nordic Journal of African Studies, 11(2), 13-13.

D’Andrea, F. M., Wormsley, D. P., & Savaiano, M. E. (2014). Unified English Braille in the United States: A research agenda for transition and instruction. International review of research in developmental disabilities, 46, 145-175.

Mwangi, D. (2014). Unukuzi wa Maandishi ya Breili katika Kiswahili. Chuo Kikuu cha Kenyatta (Unpublished Thesis).

Travers, R. M. W. (1978). An introduction to educational research.Collier-Macmillan.

Kizuka, Y., Oda, K., & Fujii,K. (1985). 6-7 A Hierarchical Model of Braille Reading. In Proceedings of the 23rd Convention of the Japanese Association of Special Education.

Tarehe ya Uchapishaji
18 January, 2024
Jinsi ya Kunukuu
Mwangi, D. (2024). Vikwazo vya Usimilishaji wa Ishara za Isimu katika Breili. Jarida La Afrika Mashariki La Masomo Ya Kiswahili, 7(1), 28-38. https://doi.org/10.37284/jammk.7.1.1699