Kubainisha Usawiri wa Ukahaba naWahusika Makahaba katika Riwaya ya Nyota ya Rehema na Ndoto ya Almasi

  • Karuhanga Deusdedit Chuo Kikuu cha Maseno
  • Florence Indede, PhD Chuo Kikuu cha Maseno
  • Deborah Nanyama Amukowa, PhD Chuo Kikuu cha Maseno
Keywords: Ukahaba, Ngono, Kuwadi, Madanguro
Sambaza Makala:

Ikisiri

Utafiti huu ulichunguza ukahaba  katika riwaya ya Nyota ya Rehema (Mohamed S.Mohamed) na Ndoto ya Almasi (Ken Walibora). Kitendo cha ukahaba kimesababisha mashaka mengi sana katika maisha ya mwanadamu kama vile kupoteza ujira, uharibikaji wa ndoa maradhi ya zinaa, vifo, kukata tamaa na utengano miongoni mwa wanajamii. Madhumuni ya utafiti huu yalikuwa ni: kubainisha usawiri wa ukahaba na wahusika makahaba katika riwaya ya Nyota ya Rehema na Ndoto ya Almasi; Mtafiti alitumia nadharia ya utekelezi ambayo ni miongoni mwa nadharia nyingi zenye mtazamo wa kisosholojia. Nadharia ya utekelezi imeendelezwa na wanasosholojia kama vile TalcortParsons na EmileDurkheim kama wanavyonukuliwa na WorselyIntroductiontoSociology (1970), huku akisema kwamba ukahaba husababishwa na mambo mawili yaani haja ya kutekeleza mahitaji ya kiuchumi na kwa kukidhi matashi ya nafsi zao kiashki.  Mtafiti pia alitumia nadharia ya umaksi iliyoanzishwa na Karl Marx (1818-1863) na FredrichEngles(1820-1895).  Nadharia hii hufaa utafiti huu kwa kudhihirisha wahusika wanaoshiriki katika vitendo vya ukahaba kwa ajili ya kupata fedha au zawadi. Mabepari au walionacho huwa na lengo la kuridhisha miili yao tu na wanyonge huwa na lengo la kupata pesa ili kutimiza mahitaji yao, pengine, mnyonge hutolea mwili wake kwa ajili ya kupewa kazi au kupandishwa cheo kazini au kama njia ya kuilinda kazi yake ili asipigwe kalamu. Utafiti huu ni wa maktabani kwa hivyo, maktaba yaliyotumika ni yale ya Chuo Kikuu cha uislamu kilichopo nchini Uganda, Chuo kikuu cha Kimataifa Metropolitan, na maktabani ya shule ya upili Heritage. Data za utafiti huu zilikusanywa kutoka maktabani kwa kutumia mbinu ya usomaji makini na uchunguzaji wa riwaya teule yaani: ile ya Nyota ya Rehema na ya Ndoto ya Almasi kwa kuzisoma na kuzichambua kwa kina na kuiwasilishwa data kwa mbinu ya kiuthamano. Utafiti huu umebainisha kuwa wahusika hufanya ukahaba ili kupata pesa au kuridhisha matashi ya nafsi zao kiashiki. Utafiti huu utakuwa wa muhimu sana kwa kufunza jamii kwamba kahaba si mwanamke peke yake kama inavyochukuliwa katika baadhi ya jamii bali kahaba ni mtu yeyote awe mwanamume au mwanamke anayeshiririki vitendo vya uzinzi

Upakuaji

Bado hatuna takwimu za upakuaji.

Marejeleo

Bakwesegha, C. (1982). ProfilesofUrbanProstitution. A casestudyfrom Uganda. (Kenya Literature Bureau, Nairobi).

Ken. Walobora. (2006), Ndoto ya Almasi.(Moran EastAfricapublishers Limited

Kezilahabi, E. (1971). RosaMistika. (East African Literature Bureau).

Kishtainy, K. (1982), The ProstituteinProgressiveAliterature. AlalinsonandBusby Ltd:

Kothari, C. R (2004) ResearchMethodology: MethodsandTechniques. New Age International (P). New Delhi India.

Lowry, R.P. (1974), SocialProblems: A CriticalAnalysisofTheoriesandPublicPolicy.

Mwandishi wa Kike na wa Kiume Uchunguzi Katika Riwaya Teule”. Tasnifu ya M. A. Kiswahili .Chuo Kikuu cha Dar es Salaam.

Madumulla, J. S. (1987). “Maendeleo ya Wahusika katika Riwaya ya Kiswahili Tanzania”, ktk: Kiswahili . Dar es Salaam:TUKI.

Mbah,F.U (1979) Ukahaba katika Tanzania Tasnifu ya Uzamili Chuo Kikuu cha Dar es salaam

Mbilinyi, M. (1983), Mwanamke wa Tanzania:AnalyticalBibliography. (MotalaCrafisika, Sweden).

Mlacha, S.A.K. (1984), “Riwaya za Visiwani (1970-1980) na Ujenzi wa Jamii Mpya”, katika Mualika. Dar es Salaam: TUKI.

Mlacha, S.A.K. (1993), Kiswahili NovelsandSociety.Dar es Salaam University Press.

Mohamed, M.S. (1972), KIU. (East African Publishing House). (1976). Nyota ya Rehema. (OxfDrd University Press).

Mohamed, S.A. (1977), Asali Chungu. (Shungwaya Publishers Limited, Nairobi). 132

Muga, E. (1980), StudiesinProstitution: East, West and South Africa, Zaire andNaveda. Kenya Literature Bureau: Nairobi.

Nguma, N. (2001), Taswira ya Mwanamke Jinsi Ilivyochorwa Katika Riwaya ya Kezilahabi. Tasnifu ya uzamili, Chuo Kikuu cha Dar es Salaam.

Saumu Juma Khamis (2017), katika utafiti wake; Kuchunguza ukahaba katika riwaya ya Kiswahili ; mifano katika Nyota ya RehemanaNdoto ya Almasi.

Senkoro, F.E. M.K. (1982), Ukahaba katika fasihi ya Kiafrika. (Tanzania Publishing House, Dar es Salaam).

Shafi, S. A. (1999), Vuta N’kuvute. Dar es Salaam. Oxford University Press.

Smart, C. (1976), Women, CrimeandCriminology. (RoutledgeandKegan Paul).

Strobel, M.N. (1975), Mwanamke mwislamu mjini Mombasa, Kenya 1966-1973. (Tasnifu ya Ph.D., Chuo Kikuu Cha California, Los Angeles).

TUKI (2004), Kamusi ya Kiswahili Sanifu. Nairobi: Oxford University Press

Tarehe ya Uchapishaji
28 December, 2022
Jinsi ya Kunukuu
Deusdedit, K., Indede, F., & Amukowa, D. (2022). Kubainisha Usawiri wa Ukahaba naWahusika Makahaba katika Riwaya ya Nyota ya Rehema na Ndoto ya Almasi. Jarida La Afrika Mashariki La Masomo Ya Kiswahili, 5(2), 155-173. https://doi.org/10.37284/jammk.5.2.1005