Mikakati ya Udumishaji wa Lugha ya Kishona Nchini Kenya

  • Mercy Moraa Motanya Chuo Kikuu cha Kenyatta
  • Boniface Ngugi Chuo Kikuu cha Kenyatta
  • Stephen Njihia Kamau Chuo Kikuu cha Kenyatta
Keywords: Udumishaji wa lugha, Uzalishaji Kijamii, Mikakati, Shinikizo, Jamiilugha, Uhamaji
Sambaza Makala:

Ikisiri

Makala haya yanalenga kuchunguza mikakati mbalimbali inayotumiwa na Washona katika kudumisha lugha ya Kishona nchini Kenya. Washona ni Wabantu ambao asili yao ni nchi ya Zimbabwe na walifika nchini Kenya kuanzia mwaka wa 1959 kwa lengo la kuhubiri injili kupitia kwa dhehebu la Gospel of God. Washona wametagusana na jamiilugha mbalimbali nchini Kenya hasa katika kaunti ya Kiambu iliyo na hali ya wingilugha hasa kwenye mitaa ya Kinoo, Kikuyu, Kiambaa, Gitaru, na Githurai ambayo ni makazi ya Washona wengi wanaoishi nchini Kenya. Mtagusano wa lugha mbalimbali waweza kuhatarisha uthabiti wa kiisimujamii wa lugha ambayo ina idadi ndogo ya wazungumzaji na ambayo haina usaidizi kutoka asasi mbalimbali za kiserikali. Hali hii ndiyo inayoikabili jamiilugha ya Washona nchini Kenya. Makala haya yaliongozwa na nadharia ya uzalishaji kijamii ya Bourdieu (1977) ambayo iliendelezwa na O’Riagain (1994). Kupitia kwa mhimili wake wa kwanza unaosema kwamba kila kizazi hubuni na kuweka mikakati ya kurithisha kizazi kinachofuata utamaduni wake, nadharia hii inasisitiza mikakati ambayo jamiilugha huweka ili kudumisha lugha ambayo ni kipengele muhimu cha utamaduni. Utafiti huu ulifanyikia maktabani na nyanjani. Utafiti wa nyanjani ulifanyikia kwenye maeneo ambayo wanajamiilugha wa Kishona huishi ili kupata data iliyobainisha mikakati ambayo Washona wanatumia ili kudumisha lugha yao ya Kishona nchini Kenya. Jumuiya ya utafiti ilikuwa jamiilugha ya Washona wanaoishi katika mitaa mitano ya kaunti ya Kiambu. Sampuli ya utafiti huu iliteuliwa kimaksudi na kwa njia elekezi. Mbinu zilizotumiwa katika ukusanyaji wa data ni mahojiano, uchunzaji na mijadala ya vikundi vidogovidogo. Data iliyokusanywa ilichanganuliwa kwa kutumia mbinu changamano. Matokeo yaliwasilishwa kwa njia ya maelezo na kuongozwa na nadharia ya uzalishaji kijamii. Kufuatia juhudi za UNESCO za kudumisha lugha asilia, utafiti huu ni wa manufaa kwa Washona wenyewe, taifa la Kenya na mataifa mengine kwa kuwa uliongezea data muhimu katika kuhifadhi lugha ya Kishona nchini Kenya

Upakuaji

Bado hatuna takwimu za upakuaji.

Marejeleo

Americans. International journal of the sociology of language, (69), 59-71.

Australian Bureau of Statistics (2016) Language of Migrants. Accessed 15/12/2022

Baker, C. (1992). Attitudes and language. Clevedon, UK: Multilingual Matters.

Baker, C. (2011). Foundations of Bilingual Education and Bilingualism. Bilingual Education & Bilingualism. Multilingual Matters.

Batibo, H. M. (2005). Language Decline and Death in Africa. Causes, Consequences and challenges, Toronto: Multilingual Matters Ltd.

Benrabah, M. (2004). Language and politics in Algeria. Nationalism and ethnic politics, 10(1), 59-78.Chambers, J. na Natalie, S. (2013) The Handbook of Language Variation and Change (ed) Malaysia: Ho printing (M) Sdn Bhd

Best, W. na Kahn, J. (2010). Research in Education, New Jersey U.S.A: Person Prentice.

Clayne, M. (2003). Towards a more language-centred approach to plurilingualism. Multilingual Matters, 43-55.

Clyne, M. G. (2005). Australia's language potential. University of New South Wales Press.

Clyne, M., & Kipp, S. (1999). Pluricentric Languages in an Immigrant Context: Spanish, Arabic and Chinese.

Demos, V. (1988). Ethnic mother-tongue maintenance among Greek Orthodox

Denzin, K. na Lincoln, Y. (2011). The SAGE Handbook of Qualitative Research. U.S.A: SAGE Publication, Inc.

Ehala, M. (2010). Ethnolinguistic vitality and intergroup processes1. Multilingual, 29, 203221.

Fishman J.(1989).‟Language and Ethnicity in minority sociolinguistic perspective” Multilingual Matters. Philadelphia: Clevedon.

Fishman, J. (1991). Reversing Language Shift: Theoretical and Empirical Foundations of Assistance to Threatened Languages. Clevedon: Multilingual Matters Ltd.

Fishman, J. A. (2000). Language planning for the “other Jewish languages” in

Gomaa, Y. A. (2011). Language maintenance and transmission: The case of Egyptian Arabic in Durham, UK. International Journal of English Linguistics, 1(1), 46.

Hildebrandt, K. A. (2004). A grammar and glossary of the Manange language. In Tibeto-Burman languages of Nepal: Manange and Sherpa. Pacific Linguistics.

Holmes, J. (2001). An introduction to sociolinguistics. New York; Harlow, Eng: Longman.

Israel: An agenda for the beginning of the 21st century. Language Problems and Language Planning, 24(3), 215-231.

Kedrebeogo, G. (1998). Language maintenance and language shift in Burkina Faso: The case of the Koromba.

Kenya Human Rights Commission (KHRC). 2019. African Missionaries in Identity Limbo: The Shona People of Kenya. KHRC

Landweer, L. (2000). Indicators of Ethno Linguistic Vitality’. Notes on Sociolinguistics pg 5 – 22 [ Online:http//www.s.l. org /socialx/ndg-lg-indicators.html]

Letsholo, R. (2009). Language maintenance or shift? Attitudes of Bakalanga youth towards their mother tongue. International Journal of Bilingual Education and Bilingualism, 12(5), 581-595.

Lune, H., Pumar, E. S., na Koppel, R. (Eds.). (2010). Perspectives in Social Research Methods and Analysis: a reader for sociology. Sage.

McCarty, T. L., na Watahomigie, L. J. (2004). Language and literacy in American Indian and Alaska Native communities. In Sociocultural contexts of language and literacy (pp. 89-120). Routledge.

McDuling, A., na Barnes, L. (2012). What is the future of Greek in South Africa? Language shift and maintenance in the Greek community of Johannesburg. Language Matters, 43(2), 166-183.

Michieka, M. (2012). Language maintenance and shift among Kenyan university students. In Selected Proceeding of the 41st Annual Conference on African Linguistics, ed. Bruce Cornell and Nicholas Rolle (pp. 164-170).

Milroy, L. (1987). Language and social networks. Oxford: Basil Blackwell.

Mulinya, D. (2020, Desemba 30). Shona Celebrate Kenyan Citizenship as Decades of Closed Legal Doors Open. Citizenship Rights in Africa Initiative.

Namei, S. (2012). Iranians in Sweden: A study of language maintenance and shift. Edita Västra Aros.

Ndubi, M. (2017, November 7). The Shona: A stateless community in Kenya yearning to gain citizenship. UNHCR Kenya. https://www.unhcr.org/ke/12739-shona-stateless-community-kenya-yearning-gain-citizenship.html

Nettle, D., na Romaine, S. (2000). Vanishing voices: The extinction of the world's languages. Oxford: Oxford University Press.

Nonaka, A. M. (2009). Estimating size, scope, and membership of the speech/sign communities of undocumented indigenous/village sign languages: The Ban Khor case study. Language & Communication, 29(3), 210-229.

O’Riagain, P. (1994). Language maintenance and language shift as strategies of social reproduction. Journal of Multilingual and Multicultural Development 15(2&3): pp. 179-197

Obiero, O. J. & Matu, P.M. (2013) Appliction of the Vitality Test on Small Languages: The Case of Suba in Kenya. The African Review: A Journal of African Politics, Development and International Affairs, 40(1), 179-202.

Orodho, J. (2004). Elements of Educational Research and Social Science Research Methods. Nairobi: Masola Publishers.

Pauwels, A. (2005). Maintaining the community language in Australia: Challenges and roles for families. International journal of bilingual education and bilingualism, 8(2-3), 124-131.

Ralli, A. (2001). Morphology in language contact: verbal loanblend formation in Asia Minor Greek (Aivaliot). Morphologies in contact (Studia Typologica). Berlin: Academie Verlag, 185-201.

Richards, C. J., & Schmidt, R. (2002). Longman Dictionary of Language Teaching and Applied Linguistics 3rd edition.

Romaine, S. (1994). Hawai'i Creole English as a literary language. Language in Society, 23(4), 527-554.

Sallabank, J. (2010). Language documentation and language policy. Language Documentation and Description, 7, 144-171.

Sangili, N. N. K. (2019). Udumishaji wa lugha ya kimaragoli katika eneobunge la uriri, Kenya (Doctoral dissertation).

Stoessel, S. (2002). Investigating the role of social networks in language maintenance and shift. International Journal of the Sociology of Language, 2002(153).

Thomason, S. G. (2000). Linguistic areas and language history. In Languages in contact (pp. 311-327). Brill.

UNESCO (2003). Language vitality and endangerment: UNESCO ad hoc expert group on endangered languages. Paris: UNESCO.

Van Aswegen, K. (2008). The maintenance of Maale in Ethiopia. Language Matters, 39(1), 29-48.

Velázquez, I. (2012). Mother's social network and family language maintenance. Journal of Multilingual and Multicultural Development, 34(2), 189-202.

Wagalla, S. (2019). Citizens or Refugees? The Case of the Shona in Kenya (1962-2017) (Doctoral dissertation, University of Nairobi).

Wolck, W. (2004). Universals of language maintenance, shift and change. Collegium antropologicum, 28(1), 5-12.

Tarehe ya Uchapishaji
14 March, 2024
Jinsi ya Kunukuu
Motanya, M., Ngugi, B., & Kamau, S. (2024). Mikakati ya Udumishaji wa Lugha ya Kishona Nchini Kenya. Jarida La Afrika Mashariki La Masomo Ya Kiswahili, 7(1), 137-154. https://doi.org/10.37284/jammk.7.1.1824