Tamathali za Usemi, Mbinu Rejeshi na Taswira katika Utenzi wa Vita vya Uhud
Ikisiri
Katika makala hii, tutaangazia jinsi tamathali za usemi, mbinu rejeshi pamoja na taswira vilivyotumika katika kuwasilisha ujumbe wa mtunzi wa utenzi wa vita vya Uhud. Utafiti wetu utaongozwa na lengo moja ambalo ni kubainisha ufaafu wa vipengele vya kimtindo kama tulivyovitaja kwenye mada yetu hapo juu katika ufumaji wa utenzi wa vita vya Uhud. Tumeelezea kila kipengele tajwa na kubainisha umuhimu wake katika utunzi wa utenzi wa vita vya Uhud. Nadharia ya umtindo ndiyo inayoongoza utafiti wetu kwani kwa maoni yetu, ndiyo itakayotufafanulia zaidi jinsi vipengele hivi vya kimtindo vimetumika katika uwasilishaji wa dhamira na maudhui ya mtunzi wa utenzi wa vita vya Uhud. Mihimili iliyohusu utafiti wetu ndiyo iliyozingatiwa katika kuongoza utafiti wetu. Vipengele tajwa vya kimtindo japo vimezamiwa na watafiti wengi wa fasihi, kipera cha ushairi hakijazamiwa sana. Tafiti ambazo tulizipitia zimekirejelea kwa njia ya juu juu. Kutokana na hali hii, utafiti wetu umelenga kuangazia vipengele hivi kwa kina ili kubainisha umuhimu wake katika kazi za kisanii, si tu katika kazi za kinadhari bali pia kwenye kazi za kishairi. Katika utafiti wetu, tutaangazia utenzi wa vita vya Uhud namna ulivyonakiliwa na Chum (1970). Kwa mtazamo wetu, vipera vingine vya kifasihi vimeangaziwa zaidi na wasanii wengi ilhali kipera cha ushairi hakijazingatiwa mno. Utafiti huu unalenga kuwapa motisha wasomi na wahakiki mbalimbali kuzamia kazi za tenzi na kuzihakiki kama vipera vingine vya kifasihi
Upakuaji
Marejeleo
Chimerah, R., & Njogu, K., (1999), Ufundishaji wa Fasihi, Nadharia na Mbinu: Nairobi: Jomo Kenyatta Foundation Ltd.
Chum, H. (mha.) (1970)., Utenzi wa vita vya Uhud: Dar es Salaam. East African Literature Bureau.
Hamad, A. M. (2017). ''Muundo wa Lugha katika Mashairi ya-Watungaji Wateule wa Zanzibar.''Tasnifu ya Uzamifu. Chuo Kikuu cha Taifa cha Zanzibar. (Haijachapishwa).
King’ei, K., & Kemoli, A. (2001). Taaluma ya Ushairi. Nairobi: Acacia Stantex Limited.
Kuvuna, S. M., na wengine. (1992). Nuru ya Ushairi: Mwongozo na Uchambuzi. Nairobi. Kenya Literature Bureau.
Mbatiah, M. (2001). Kamusi ya Fasihi. Nairobi. Standard Textbooks Graphics and publishing.
Mohammed, S. A. (1995). Kunga za Nathari ya Kiswahili: Riwaya, Tamthilia na Hadithi Fupi. Nairobi: East African Educational Publishers.
Murungi, G. K. (2013). ''Mtindo Unavyoendeleza Maudhui katika Natala.'' Tasnifu ya Uzamili. Chuo Kikuu cha Nairobi. (Haijachapishwa)
Ndumbu, J. M. (2013). Matumizi ya takriri na sitiari katika Utenzi wa Rasi'l ghuli. Tasnifu ya Uzamili Chuo Kikuu cha Nairobi. (Haijachapishwa).
Wamitila, K. W., (2008), Kanzi ya Fasihi: Misingi ya Uchanganuzi wa Fasihi. Nairobi: Focus Publications Ltd.
Wamitila, K. W. (2003), Kichocheo cha Fasihi: Simulizi na Andishi: Nairobi. Focus Publications.
Copyright (c) 2022 Dickens Bonyi Obwogi
This work is licensed under a Creative Commons Attribution 4.0 International License.