Uchambuzi wa Hali ya Ukatili wa Wanyama Katika Mashamba Nchini Kenya

  • Maureen K. Luvanda, PhD Kenya Agricultural & Livestock Research Organisation
Keywords: Ustawi wa Wanyama, Ukatili wa Wanyama, Maadili, Kenya, Wakulima, Wanyama
Sambaza Makala:

Ikisiri

Hati hii imetayarishwa kushughulikia maswala ya ustawi wa mifugo nchini Kenya na kuongezeka kwa ujuzi wa wafanyikazi wa mstari wa mbele kuhusiana na swala la viwango na sheria zinazoongoza ustawi wa wanyama. Lengo kuu lilikuwa kutathmini vipengele vya utunzaji wa wanyama, matibabu na ujuzi wa ustawi wa wanyama miongoni mwa wakulima nchini Kenya. Tuligundua ya kwamba wakulima wengi hawaelewi kimsingi ustawi wa wanyama kwa kuwa wengi wao hawajapata mafunzo maalum na wengi wao hawajui sheria zilizopo kuhusu mada hiyo. Wadau wengine walitathminiwa pia kwa madhumuni ya kulinganisha na madaktari wa mifugo na kama ilivyotarajiwa walikuwa na ujuzi zaidi kuhusu ustawi wa wanyama na desturi zinazoikuza. Hata hivyo, kadhaa walionelea kwamba serikali haikuweka juhudi za kutosha katika kukuza ufahamu wa umma au hata kuhamasisha jamii dhidi ya ukatili wa wanyama. Kulingana na maelezo yaliyopatikana, hati hii iliundwa ili kutoa suluhisho ya vitendo linapohusu swala la kuongeza ustawi wa wanyama nchini Kenya. Mapendekezo haya ni pamoja na kuishinikiza serikali kuanzisha sera madhubuti dhidi ya ukatili wa wanyama, kuwahimiza maafisa wa sheria kutekeleza sheria za sasa kwa kutumia mifumo ambayo tayari iko na kuhimiza mazungumzo ya jamii na ushiriki wa moja kwa moja wa watu walio mstari wa mbele.

Upakuaji

Bado hatuna takwimu za upakuaji.

Marejeleo

Alarcon, P., Fèvre, E. M., Muinde, P., Murungi, M. K., Kiambi, S., Akoko, J., & Rushton, J. (2017). Urban livestock keeping in the city of Nairobi: diversity of production systems, supply chains, and their disease management and risks. Frontiers in Veterinary Science, 4, 171.

Broom, D. (1991). Animal Welfare: Concepts and Measurements. Journal of Animal Science, 69(10), 4167-4175.

Edwards-Callaway, L. N. & Calvo-Lorenzo, M. S. (2020). Animal Welfare in the US slaughter industry - a focus on fed cattle. Journal of Animal Science, 98(4).

Greger, M. & Koneswaran, G. (2010). The public health impacts of concentrated animal feeding operations on local communities. Fam Community Health, 33(1), 373-382.

Greger, M. (2007). The long haul: risks associated with livestock transport. Biosecurity and bioterrorism: biodefense strategy, practice, and science, 5(4), 301-312. doi: 10.1089/bsp.2007.0028

Greger, M. (2011). Transgenesis in animal agriculture and zoonotic disease resistance. CAB Reviews: Perspectives in Agriculture, Veterinary Science, Nutrition & Natural Resources, 6(41).

Kimwele, C., Matheka, D., & Ferdowsian, H. (2011). A Kenyan perspective on the use of animals in science education and scientific research in Africa and prospects for improvement. Pan African Medical Journal, 9(1).

Manning, J., Power, D., & Cosby, A. (2021). Legal Complexities of Animal Welfare in Australia: Do On-Animal Sensors Offer a Future Option?. Animals, 11(1), 91.

Mogoa, E. G., Wabacha, J. K., Mbithi, P. M., & Kiama, S. G. (2005). An overview of animal welfare issues in Kenya. Kenya Veterinarian, 29, 48-52.

Molomo, M., & Mumba, T. (2014). Drivers for animal welfare policies in Africa. Revue Scientifique et Technique (International Office of Epizootics), 33(1), 47-53.

Njisane, Y. Z., Mukumbo, F. E., & Muchenje, V. (2020). An outlook on livestock welfare conditions in African communities—A review. Asian-Australasian Journal of Animal Sciences, 33(6), 867-878.

OIE – Terrestrial Animal Health Code. (2019). Section 7: Animal Welfare, Chapter 7.1: Introduction to the recommendations for animal welfare”, 7.1.1-7.1.5

Rioja-Lang, F.C., et al. (2020). Prioritization of Farm Animal Welfare Issues Using Expert Consensus. Frontiers in Veterinary Science, 6(495).

Russel, W., & Burch, R. (1959). The Principles of Humane Experimental Technique; as reprinted 1992. Universities Federation for Animal Welfare: Wheathampstead, UK.

Thornton, P. K. (2010). Livestock production: recent trends, future prospects. Philosophical Transactions of the Royal Society B: Biological Sciences, 365(1554), 2853-2867.

Thumbi, S. M., Njenga, M. K., Marsh, T. L., Noh, S., Otiang, E., Munyua, P., ... & McElwain, T. F. (2015). Linking human health and livestock health: a “one-health” platform for integrated analysis of human health, livestock health, and economic welfare in livestock dependent communities. PloS one, 10(3), e0120761.

Tarehe ya Uchapishaji
19 April, 2022
Jinsi ya Kunukuu
Luvanda, M. (2022). Uchambuzi wa Hali ya Ukatili wa Wanyama Katika Mashamba Nchini Kenya. Jarida La Afrika Mashariki La Masomo Ya Kiswahili, 5(1), 49-63. https://doi.org/10.37284/jammk.5.1.626