Athari za Mtagusano Kati ya Jamii na Ekolojia Katika Ushairi wa Mberia: Bara Jingine na Rangi ya Anga
Ikisiri
Makala haya yameangazia athari za mtagusano kati ya jamii na ekolojia katika diwani ya Bara Jingine na Rangi ya Anga. Ili kufaulisha hili, tumeongozwa na nadharia ya Ekolojia ambayo inaangazia mahusiano na mwingiliano kati ya jamii na mazingira inamoishi. Nadharia hii ya Ekolojia inahusishwa na Cheryll Glotfelty na Harold Fromm mwaka wa 1996. Malengo ya uchunguzi wetu ni kubainisha athari za mtagusano kati ya jamii na mazingira ya kiasili katika diwani ya Bara Jingine na Rangi ya Anga. Baada ya uchunguzi wetu tumebainisha kuwa wanajamii wanapotagusana na mazingira wanachangia katika uharibifu wa misitu, hewa, mito, mabwawa na udongo. Hali hii inaathiri mataifa husika kiuchumi kwani binadamu huishi katika mazingira haya. Isitoshe, mazingira haya huwa ndio makazi ya wanyama na viumbe vingine ambavyo huwa na wajibu mkubwa katika mchakato mzima wa ekolojia. Ili kubainisha haya tumechanganua data yetu kwa njia ya maelezo huku tukitoa ufafanuzi na thibitisho kutoka katika diwani ya Bara jingine na Rangi ya Anga.
Upakuaji
Copyright (c) 2019 John Mugwe Mwaniki, Rayya Timammy, PhD, Mary Ndung'u
This work is licensed under a Creative Commons Attribution 4.0 International License.