https://journals.eanso.org/index.php/eajss/issue/feedEast African Journal of Swahili Studies2025-10-24T13:25:03+00:00Prof. Jack Simonseditor@eanso.orgOpen Journal Systems<p>The development of Swahili as a language is important in the development and preservation of indigenous culture, knowledge and religion in Swahili speaking regions in Africa. This peer-reviewed journal therefore exclusively published only Swahili articles. The articles publishable under this journal range from all genres of knowledge provided that they are written in Swahili language. Authors submitting to this journal can however decide to translate their articles into English and publish the translations in any other of our hosted journals.</p>https://journals.eanso.org/index.php/eajss/article/view/3247Mabadiliko katika Mtaala wa Elimu ya Msingi na Namna Yanavyoathiri Tathmini katika Elimu ya Juu2025-07-02T15:51:34+00:00Jackline Osagi Mwanzijacklinemwanzi@yahoo.com<p>Makala haya yamekusudia kuchunguza namna ambavyo mabadiliko katika mtaala wa elimu ya msingi yanavyoathiri tathmini katika elimu ya juu. Mabadiliko ya mtaala yanafanyika katika ngazi ya kitaifa nchini Kenya ambapo mfumo wa elimu wa 8-4-4 unaondolewa na nafasi yake kuchukuliwa na mtaala wa umilisi (CBC). Mabadiliko haya yamejikita katika elimu ya msingi, kuanzia kiwango cha chekechea, shule za upili hadi kwenye vyuo vinavyotoa elimu ya kiufundi kote nchini. Kwa sasa, mabadiliko katika mtaala wa kitaifa hayajaathiri vyuo vikuu kunakotolewa elimu ya juu. Hata hivyo, wanafunzi wanaojiunga na vyuo vikuu huandaliwa kupitia kwa mafunzo ya shule za upili. Hivyo basi mabadiliko yoyote yanayotokea katika elimu ya msingi lazima yataathiri programu za mafunzo yanayotolewa katika vyuo vikuu. Makala haya yataangazia kipengele cha tathmini katika vyuo vikuu kwa kuzingatia mabadiliko katika mfumo wa elimu uliopo na vigezo vinavyoelekeza tathmini katika mfumo wa elimu wa umilisi. Mabadiliko katika tathmini katika mfumo wa elimu wa umilisi yanaashiria kuwepo haja ya kufanya mabadiliko sawia ya tathmini katika mafunzo ya elimu ya juu katika vyuo vikuu. Hali hii inatokea kuwa hivi kwa kuwa wanafunzi wanapojiunga na vyuo vikuu watakuwa wamezoeshwa tathmini ya shule za upili ambayo hufanyika katika kila hatua ya ujifunzaji mafunzo yanapoendelea tofauti na illivyokuwa awali ambapo tathmini ilifanyika mara moja mwishoni baada ya kipindi maalumu cha mafunzo (mwishoni mwa miaka minane katika shule za msingi na miaka minne katika shule za upili). Swali hapa ni je, tathmini ya awali iliyozoeleka na ambayo ilifanyika baada ya kipindi maalumu bado itafaa? Bado itafikia malengo yaliyopo ya elimu? Kufikia sasa, hakuna mwelekeo wowote ambao umetolewa kuhusiana na hili. Hali hii inapelekea kuwepo haja ya kubuni sera itakayotoa mwelekeo kuhusu vigezo vinavyofaa kuzingatiwa katika kubadili tathmini katika vyuo vikuu ili iendane na mabadiliko yanayoendelea kutokea katika mfumo wa elimu uliopo. Mabadiliko katika tathmini vyuoni yanaweza kufanyika kwa kulinganisha na kulinganua tathmini iliyokuwepo awali na iliyopo hivi sasa katika elimu ya msingi na vyuo vikuu. Makala haya yamechanganua changamoto zinazotokana na hiyo mifumo miwili ya tathmini na kuangazia namna ambavyo aina zote mbili za tathmini humwathiri mwanafunzi ambaye ndiye mwathiriwa mkuu. Makala haya yamelenga kuwezesha vyuo vikuu kutambua mielekeo na mitazamo ambayo wanafunzi wanaotarajiwa kujiunga navyo huingia nayo vyuoni kutokana na namna wanavyotathminiwa wanapopokea elimu ya msingi. Makala haya yametokana na uchambuzi na mapitio ya maandishi yaliyopo tayari kuhusu mifumo hii miwili ya elimu pamoja na maoni ya wataalamu wa masuala ya mitaala. Maandishi haya yalipatikana maktabani na mitandaoni.</p>2025-07-02T15:13:19+00:00##submission.copyrightStatement##https://journals.eanso.org/index.php/eajss/article/view/3248Vichocheo Vinavyowafanya Wahudumu wa Bodaboda na Abiria Kuzingatia au Kukiuka Upole Katika Mawasiliano2025-07-02T15:51:34+00:00Faith Mbithe Kathukyafaithmbithe202@gmail.comJohn Khaisie Wanyama, PhDkhaisie.john@embuni.ac.keTimothy Kinoti M’ngaruthi, PhDmngaruthi.timothy@embuni.ac.ke<p>Upole ni muhimu katika kufanikisha mawasiliano. Husaidia katika kukabiliana na matendo ya kutishia uso. Utafiti huu ulilenga kuchunguza kuhusu sababu zinazowachochea wahudumu wa bodaboda na abiria kuzingatia au kukiuka matumizi ya mikakati ya upole katika mawasiliano yao. Nadharia ya upole ndiyo iliyotumika kuelekeza utafiti huu. Utafiti ulifanyika katika kaunti ndogo ya Mbooni iliyo katika kaunti ya Makueni, nchini Kenya. Walengwa walikuwa ni wahudumu wa bodaboda na abiria walioteuliwa kimakusudi hadi pale ambapo kiwango kifu kilifikiwa. Utafiti huu wa kithamano, ulitumia mbinu ya uchunzaji na mahojiano katika kukusanya data. Uchanganuzi wa kimaudhui ulitumika ili kuhakiki majibu ya mahojiano kwa kuelekezwa na mihimili ya nadharia. Matokeo ya utafiti yalionyesha kuwa kuna sababu kadhaa zinazochochea hali ya kuzingatia au kukiuka matumizi ya mikakati ya upole katika mawasiliano. Sababu hizo ni kama vile: faida tarajiwa, tofauti za mahusiano, haja ya kutaka kuonyesha heshima kwa sababu ya tofauti za kimamlaka na hali ya kutaka kukabiliana na uzito wa tendo la kutishia uso. Faida au matokeo tarajiwa yalichochea uzingatiaji wa mikakati ya upole sana. Sababu hii ilijitokeza kwa wingi kwani mawasiliano yalitokea katika muktadha wa uchukuzi ambapo mantiki huzingatiwa sana ili kufikia malengo ya kibiashara. Hivyo, wahudumu wa bodaboda na abiria walizingatia zaidi mafanikio ya mawasiliano kuliko vipengele vya kijamii. Matokeo ya utafiti huu yanaiarifu nadharia kwani yanaonyesha kuwa mbali na vigezo vya kijamii vinavyosisitizwa na nadharia, faida tarajiwa huchochea matumizi ya mikakati ya upole katika muktadha wa uchukuzi. Utafiti huu una umuhimu kwa taaluma ya mawasiliano hasa kwa kurahisisha maingiliano baina ya watu katika jamii. Isitoshe utakuwa wenzo muhimu kwa watafiti wa baadaye watakaojihusisha na uga wa pragmatiki</p>2025-07-02T15:19:46+00:00##submission.copyrightStatement##https://journals.eanso.org/index.php/eajss/article/view/3256Utafiti wa Lahaja Kupitia Macho ya Jamii: Matumizi ya Mtazamo Tambuzi wa Elimu Lahaja Katika Kaunti ya Lamu2025-07-03T14:48:31+00:00Judy Wangari Onyanchajudynyamweya16@uonbi.ac.keRayya Timammyrayya@uonbi.ac.keMungai Mutonyammutonya@wustl.edu<p>Utafiti huu unachunguza uainishaji wa mipaka ya lahaja za Kiswahili zinazozungumzwa katika Kaunti ya Lamu, Kenya, kwa kutumia nadharia ya Mtazamo Tambuzi wa Elimu Lahaja (Preston, 1989). Tofauti na tafiti za awali zilizozingatia vipengele vya kimuundo vya lugha, utafiti huu umejikita katika maoni, mitazamo, uelewa na hisia za wasemaji wazawa kama vigezo halali vya kutambua na kuainisha lahaja. Kwa kutumia mbinu ya uchoraji wa ramani za mikono, sauti zilizorekodiwa, na mijadala ya vikundi, washiriki waliainisha maeneo ya lahaja kwa msingi wa tajriba zao binafsi. Data hiyo ilichakatwa kwa kutumia teknolojia ya GIS (QGIS na ArcGIS) kwa njia ya <em>Kernel Density Estimation</em> (KDE). Matokeo yameonyesha kuwepo kwa makundi makuu manne ya lahaja: Kiamu, Kipate, Kisiu na Kitikuu, huku Kishela na Kimatondoni zikiwa kwenye hatari ya kufifia kutokana na ushawishi wa Kiamu. Aidha, vipengele vya kifonolojia, kimofolojia na kisintaksia vilijitokeza kuwa msingi wa utambuzi wa tofauti hizo. Imebainika kuwa asili ya mzungumzaji, uzoefu wa lugha, na uhusiano wa kijamii ni vigezo muhimu vinavyoathiri namna wanavyotambua na kuchora mipaka ya lahaja. Utafiti huu unatoa mchango mpya kwa taaluma ya isimu-jamii na lahaja kwa kusisitiza umuhimu wa data tambuzi kutoka kwa jamii, na hivyo kupanua upeo wa utafiti wa lugha za Kiafrika kutoka katika mtazamo wa jamii kuelekea usomi wa kitaaluma</p>2025-07-03T13:59:28+00:00##submission.copyrightStatement##https://journals.eanso.org/index.php/eajss/article/view/3257Unyanyasikaji wa Wanaume katika Diwani za Tumbo Lisiloshiba na Maskini Milionea na Hadithi Nyingine2025-07-03T14:48:31+00:00Elizabeth Wanjiru Waithakaewwanjiru84@gmail.comJohn Khaisie Wanyama, PhDkhaisie.john@embuni.ac.keTimothy Kinoti M’ngaruthi, PhDmngaruthi.timothy@embuni.ac.ke<p>Fasihi kama kioo cha jamii hutumia lugha kwa ufanifu mkubwa kutuchorea taswira kamili ya yale yanayotendeka katika jamii. Fasihi haizuki katika ombwe tupu. Hivyo basi utafiti huu ulichunguza unyanyasikaji wa wanaume katika jamii. Ulichunguza suala mtambuko ambalo linaathiri haki za wanaume kama inavyosawiriwa katika Diwani ya Tumbo Lisiloshiba na Hadithi Nyingine iliyohaririwa na Alifa Chokocho na Dumu Kayanda na Maskini Milionea na Hadithi Nyingine iliyohaririwa na Ken Walibora. Lengo kuu la makala hii ni kuchunguza namna wanaume hunyanyasika katika diwani teule. Ilikuafikia lengo hili, nadharia ya Mtagusano wa Vitambulisho ilitumiwa. Ni mojawapo ya nadharia za kijinsia. Utafiti huu ulikuwa wa kimaktaba. Data ya utafiti ilikusanywa kwa kusoma hadithi teule kutoka diwani za Kiswahili zilizoteuliwa vitabu, majarida na makala mengine kutoka mitandaoni. Uteuzi wa sampuli ulikuwa wa kimaksudi. Data iliyokusanywa ilichanganuliwa kimaelezo kwa kutumia mbinu ya uchanganuzi matini ikiongozwa na madhumuni ya utafiti. Matokeo ya utafiti yaliwasilishwa kwa njia ya kimaelezo. Matokeo ya makala yalionyesha kuwa mwanamume hunyanyasika kwa namna nyingi kama vile: kula uroda nje ya ndoa, utengano wa kijamaa, kukataliwa uchumba, upyaro, kunyimwa chakula na kuchapwa. Vipengele vya utambulisho vinavyoshirikiana na kusababisha unyanyasikaji wa wanaume ni: uchumi, jinsia, tabaka, matarajio ya kijamii. Kipengele kinachosababisha unyanyasikaji wa wanaume zaidi ni kipengele cha uchumi. Uchunguzi huu utawafaa wasomi, wanajamii, na waandishi kwani watapata uelewa zaidi wa aina za unyanyasikaji unaotendewa wanaume na kutafuta mbinu za kuwaokoa kutoka kwa udhalimu huu. Vile vile utakuwa na mchango katika taaluma ya fasihi ya Kiswahili.</p>2025-07-03T14:03:43+00:00##submission.copyrightStatement##https://journals.eanso.org/index.php/eajss/article/view/3277Mbinu za Kifasihi katika Uundaji na Uhawilishaji wa Maarifa Kupitia Bembezi za Jamii ya Watumbatu2025-07-07T15:38:22+00:00Riziki Pembe Jumarizikijamal@yahoo.com<p>Makala hii inachunguza mbinu za kifasihi zinazotumika kuunda bembezi za jamii ya Watumbatu kwa lengo la kubaini mchango wake katika uhifadhi wa maarifa ya kijamii, utamaduni na maadili. Utafiti huu ulifanyika Zanzibar, ukilenga kuchambua vipengele vya kifasihi vilivyomo katika bembezi kwa kutumia Nadharia ya Fasihi Simulizi. Mbinu za ukusanyaji wa data zilihusisha mahojiano, usikilizaji wa nyimbo na uchambuzi wa matini za fasihi simulizi. Data iliyokusanywa ilichambuliwa kwa kutumia mbinu ya uchambuzi wa maudhui (Krippendorff, 2004), ambapo matokeo yanaonesha kuwa bembezi za Watumbatu zinatumia mbinu mbalimbali za kifasihi kama semi, tamathali za semi, usimulizi, vipamba-sauti, majazi na usambamba. Semi zilizotumika ni pamoja na methali, nahau na misemo inayobeba maana za kihisia na mafunzo ya kijamii, jambo linalothibitisha umuhimu wa lugha katika kujenga utambulisho wa jamii (Wamitila, 2003). Tamathali za semi kama tashbiha, sitiari na takriri huimarisha maana na mvuto wa lugha ya bembezi, huku usimulizi wa nafsi ya kwanza, pili na tatu ukitumiwa ili kuwafanya watoto washiriki na kuelewa nyimbo hizi kwa undani. Vipamba-sauti kama takriri na urari wa vina husaidia kukumbuka na kuelewa nyimbo kwa urahisi, huku majazi na usambamba vikiongeza mshikamano wa maudhui. Uchunguzi huu unathibitisha kuwa bembezi si nyimbo za kuburudisha pekee, bali ni chombo muhimu cha uhifadhi wa maarifa, uhamasishaji wa lugha na uendelezaji wa utamaduni wa jamii ya Watumbatu. Tafiti zaidi zinahitajika kuchunguza bembezi katika jamii nyingine za Kiswahili ili kubaini athari zake kwa maendeleo ya lugha na elimu ya watoto.</p>2025-07-07T15:36:56+00:00##submission.copyrightStatement##https://journals.eanso.org/index.php/eajss/article/view/3281Ujenzi wa Sifa za Mhusika wa Riwaya ya Kiswahili: Tathmini ya Mchango wa Mandhari katika Kiu na Kidagaa Kimemwozea2025-07-07T19:18:41+00:00Wyckliffe Collins Jaokowycliffe.collins@yahoo.comStanley Adika Kevogosurayangu@gmail.com<p>Mandhari hufasiliwa kuwa ni wakati na mahali patendekapo kadhia, visa au matukio katika utungo wa kifasihi unaohusika. Mandhari yanaweza kuwa halisi au ya kufikirika. Utafiti ulioichipuza makala hii uliazimia kuchunguza usawiri wa mandhari katika riwaya ya Mohamed S. Mohamed, Kiu pamoja na ile ya Ken Walibora, Kidagaa Kimwemwozea. Ingawa malengo muhsusi ya utafiti yalikuwa matatu, makala hii inazamia lengo moja tu - kutathmini mchango wa mandhari katika ujenzi wa sifa za wahusika katika riwaya ya Kiu na Kidagaa Kimemwozea. Tathmini yenyewe imekitwa kwenye mseto wa nadharia mbili - Uhalisia na Umuundo. Nadharia ya Uhalisia inachimuza uyakinifu wa mandhari ya kijamii ilhali nadharia ya Umuundo ikasisitiza dhima na uhusiano wa vipengele vya sanaa. Utafiti huu wenye mkabala wa kithamano ulifanywa maktabani kwa kuzingatia muundo wa kiuchanganuzi. Eneo la utafiti ni fasihi andishi, hususan utanzu wa riwaya ya Kiswahili. Idadi lengwa ya utafiti ni riwaya 10 za kiuhalisia zinazosawiri mandhari halisi. Sampuli ya riwaya mbili, Kiu na Kidagaa Kimemwozea, iliteuliwa kwa usampulishaji dhaminifu. Riwaya hizi ziliteuliwa kwa misingi ya wingi wa vifani vilivyochunguzwa, yaani usawiri wa mandhari. Pamoja na kuakisi malengo ya utafiti, utunzi wa riwaya teule unaambatana na mihimili ya mseto wa nadharia za utafiti. Data msingi ya utafiti ilikusanywa kwa usomaji wa kina wa matini za riwaya teule. Nazo data za upili zikakusanywa kwa usomaji wa kina wa vitabu, tasnifu na makala anuwai za kitaaluma. Data zilizokusanywa ziliainishwa kwa mujibu wa mihimili ya nadharia na malengo ya utafiti. Zilichanganuliwa kwa mujibu wa yaliyomo na matokeo kuwasilishwa kimaelezo. Matokeo ya utafiti yanadhihirisha kwamba mandhari yana mchango wa moja kwa moja katika ujenzi wa sifa za wahusika. Mandhari hayo ni kama vile: ya mahali(upembeni mwa Mto Kiberenge, chumba cha Mtemi Nasaba Bora, msituni, seli, chumba cha Mzee Mwinyi na mandhari ya mitaa kama wa vibyongoni, Selea, Ukele na mingineyo) na ya kiwakati (enzi za kikoloni,miaka mitano, Vitaa Vikuu vya Pili vya Dunia na kadhalika). Mandhari haya yalisukwa kwa ustadi ambao ulichangia ukuzaji wa sifa za wahusika kwa urahisi mno. Matokeo ya utafiti huu yana tija kwa wanariwaya na wahakiki wa kazi za kifasihi kwa jumla. Yatawasaidia kutunga visa vinavyosawiri na kuakisi mandhari kuntu. Isitoshe, wahakiki wa kazi za fasihi watawezeshwa kubaini na kutathmini mandhari anuwai pamoja na dhima zao katika kazi za kifasihi.</p>2025-07-07T19:18:00+00:00##submission.copyrightStatement##https://journals.eanso.org/index.php/eajss/article/view/3286Mikakati ya Kimtindo katika Muziki wa Benga wa Jamii ya Wakamba: Mkabala wa Umtindo2025-07-08T20:14:20+00:00Carolyne Muthini Mutukumuthinimutuku707@gmail.comJohn Khaisie Wanyama, PhDkhaisie.john@embuni.ac.keTimothy Kinoti M’ngaruthi, PhDmngaruthi.timothy@embuni.ac.ke<p>Muziki wa benga ni utanzu maarufu nchini Kenya. Hujitambulisha kwa sifa ya mdundo na mapigo ya kasi pamoja na ustadi wa msanii wa kucheza gitaa na kuimba kwa mtindo maalum. Utafiti huu ulilenga kubainisha mikakati ya mtindo inayotumika katika muziki wa benga wa jamii ya Wakamba kujenga hisia na athari za kijamii. Uchunguzi huu uliongozwa na kielelezo cha Umtindo. Umtindo hufasiri na kuhakiki tungo kwa kuzingatia mtazamo wa kiisimu kama taaluma iliyo na uhusiano wa karibu na fasihi. Uchunguzi wa kimtindo huhusisha namna lugha inavyotumika katika matini ili kujenga maana na athari. Usampulishaji ulifanywa kimakusudi ambapo nyimbo tano za muziki wa benga wa jamii ya Wakamba ziliteuliwa. Ukusanyaji wa data ulihusisha upakuaji wa nyimbo za benga kutoka kwa mtandao wa kijamii wa <em>Youtube</em> na unakili wa mishororo yake. Mbinu ya uchanganuzi matini ilitumika kubainisha mikakati ya kimtindo na kuchanganuliwa kithamano kwa kuelekezwa na mihimili ya nadharia ya umtindo. Data zilikuwa ni maneno, dhana, kauli, virai na sentensi zinazotumiwa na waimbaji wa muziki wa benga wa jamii ya Wakamba zinazohusisha vipengele vya kimtindo. Matokeo ya utafiti yaliwasilishwa kimaelezo. Ilibainika kuwa, waimbaji wa muziki wa benga wa jamii ya Wakamba hutumia mikakati ya kimtindo kama vile ugawaji wa beti, uradidi, urudiaji, tamathali za usemi na aina anui za sentensi kuwasilisha ujumbe. Utafiti huu ni muhimu katika kuufanya muziki wa benga wa jamii ya Wakamba kutambulika katika nyanja za utafiti wa kielimu wa fasihi na lugha kama kategoria ya nyimbo za kitamaduni. Utachangia taaluma ya isimu na mawasiliano kwa kuangazia baadhi ya teuzi za kiisimu zinazofanywa na wasanii</p>2025-07-08T20:13:51+00:00##submission.copyrightStatement##https://journals.eanso.org/index.php/eajss/article/view/3318Uangavu wa Maana kama Nyenzo ya Ujalizaji katika Lugha ya Kiswahili2025-07-17T07:09:24+00:00Amulike Abraham Mwampambaamulikemwampamba@gmail.comLohay Marko Labiswaimarkolabiswai964@gmail.com<p>Makala haya yanahusu uangavu wa maana kama nyenzo ya ujalizaji katika lugha ya Kiswahili. Lengo la makala haya ni kuonesha kuwa ujalizaji huwa wa lazima ili kukidhi uangavu wa maana na si kukidhi miundo pekee. Data za makala haya zimekusanywa kwa njia ya usomaji makini, kuchambuliwa kwa nadharia ya Uchambuzi wa Maudhui na kuwasilishwa kwa kutumia mkabala wa kimaelezo. Aidha, wataalamu wengi wanakieleza kijalizo kama kipashio mojawapo katika sentensi. Hata hivyo hawabainishi wazi ulazima wa kijalizo katika sentensi huukiliwa na nini. Baadhi wanataja tu kuwa kijalizo ni cha lazima katika muundo wa sentensi. Miongoni mwao ni Massamba (2004); Habwe na Karanja (2004); Koech (2013); Matei (2017); Philipo na Kuyenga (2017) na Mtego (2022). Makala yameonesha jinsi uangavu wa maana unavyokifanya kijalizo kuwa cha lazima katika sentensi za Kiswahili. Makala yamedhihirisha kuwa kijalizo huwa cha lazima si tu kukidhi miundo ya sahihi bali pia kukidhi uangavu wa maana katika sentensi za lugha. Matokeo ya makala haya yameonesha kuwa ujalizaji katika tungo si jambo la hiari bali ni hitaji la lazima. Ulazima wa ujalizaji katika tungo hutokana na ukweli kwamba ili tungo iwe na uangavu lazima pawepo ujalizaji. Kwa hiyo, mwandishi anapendekeza kwamba ujalizaji katika tungo usifanyike ili tu kukamilisha muundo wa tungo pekee bali ufanyike ili kuleta uangavu wa maana katika tungo. Kwa kuwa lengo la lugha ni kukidhi mwasiliano, tungo zenye uangavu utokanao na ujalizaji ndizo zenye uwezo wa kufikia hitajio hilo</p>2025-07-14T19:09:46+00:00##submission.copyrightStatement##https://journals.eanso.org/index.php/eajss/article/view/3334Usawiri wa Vyombo vya Dola katika Tamthilia ya Kilio cha Haki (1981) Kifo Kisimani (2001) na Upepo wa Mvua (2013)2025-07-17T08:13:51+00:00Mutegi Dolly Kendikendidolly94@gmail.comMurithi Joseph Jessekendidolly94@gmail.com<p>Vyombo vya Dola ni taasisi za serikali zilizopewa mamlaka kikatiba kutekeleza sheria na kuendesha maswala ya nchi. Usalama na ulinzi wa nchi uhakikiswa kupitia kwa taasisi hizi. Umuhimu wake katika maisha ya binadamu ni wa juu zaidi. Fasihi ni kioo cha jamii na huyasawiri mambo yaliyopo na yanayotendeka katika jamii katika ukamilifu wake. Katika makala hii tulichambua namna waandishi wa tamthilia teule wanavyozisawiri taasisi hizi katika tamthilia zao. Tulitumia mbinu ya kusoma kwa kina maktabani kukusanya data ya utafiti. Nadharia ya mabadiliko iliyoasisiwa na Kurt Lewin ndiyo iliyotuongoza katika utafiti wetu iliyotusaidia kubaini utenda kazi wa Vyombo vya Dola na mabadiliko yaliyotokea katika utendakazi wa taasisi hizi katika mpito wa wakati. Tulibainisha kuwa taasisi hizi ni dhulumu na hutumiwa kutimiza matakwa ya viongozi au serikali iliyo hatamuni badala ya kushughulia wanajamii. Taasisi hizi huishia kukiuka sheria kwa kulinda na kutunza masilahi ya kisiasa na ya kiuchumi ya watawala badala ya kutetea haki za mtu binafsi. Mabadiliko yamepatikana kwa kiasi fulani hasa baada ya kuidhinishwa kwa katiba mpya ya mwaka 2010 iliyopendekeza mageuzi mbalimbali katika taasisi hizi. Baadhi ya taasisi hizi bado ziliendeleza dhuluma, japokuwa sasa kwa njia fiche si kwa njia ya uwazi. Japokuwa mabadiliko hayajapatikana kwa ukamilifu, hatua kubwa zimepigwa na mchakato huu endelevu unazidi kutiliwa mkazo. Makala hii inapendekeza kuwepo na sheria na kanuni na njia mbadala za kuwajibisha Vyombo vya Dola ili taasisi hizi ziweze kutumikia jamii pana na kuwepo na imani na amani katika ya asasi za utawala na wanajamii. Uwajibikaji huu utasaidia kuondoa ukatili na dhuluma inayoendelezwa na taasisi hizi kwa wanajamii na kuhakikisha kuwa japokuwa vikosi hivi viko chini ya uongozi wa serikali, havitumiwi na serikali na watawala kudumisha nguvu zao za kiutawala.</p>2025-07-17T08:06:53+00:00##submission.copyrightStatement##https://journals.eanso.org/index.php/eajss/article/view/3347Maudhui ya Ukungwi katika Nyimbo Teule za Taarab2025-07-18T13:49:16+00:00Fadhili Hamisi Wendofadhiliwendo5@gmail.comKaui Titus, PhDkauititus@ku.ac.ke<p>Nyimbo za taarab zimetafitiwa na wataalam mbalimbali kwa mitazamo tofautitofauti. Kutokana na uchunguzi wa kina wa mtafiti, inabainika kuwa tafiti za awali kuhusu nyimbo za taarab, zimeegemezwa kwenye uchunguzi wa mafumbo katika taarab, masuala ya itikadi, nafasi ya mwanamke katika nyimbo za taarab usimulizi pamoja na uchanganuzi wa taswira katika nyimbo za taarab. Swala la jumbe za nyimbo za taarab kufungamana na mambo ya kijamii yakiwemo utamaduni limetajwa tu kijuujuu katika tafiti zao. Kutokana na upekuzi wa kina wa mtafiti, hakuna utafiti ambao umefanywa kuhusu dhima ya kungwi inavyotekelezwa na baadhi ya nyimbo za taarab. Utafiti huu ulihusu ubainishaji wa maudhui ya ukungwi katika nyimbo teule za taarab. Utafiti huu uliongozwa na nadharia ya Simiotiki. Nadharia hii iliasisiwa na Ferdinand Dessaussure (1983) na Charles Pierce (1998) na inahusu uhusiano uliopo kati ya kitaja na kitajwa na matumizi ya ishara, picha na msimbo. Nguzo hii ilisaidia katika kufafanua mbinu za uwasilishaji wa ujumbe katika nyimbo teule za taarab. Data ya kimsingi iliyoichanganuliwa ilikuwa ya maktabani ambapo mtafiti alipakua nyimbo teule kutoka kwenye mtandao wa You Tube na kuzichanganua kwa kina. Matokeo yalionyesha kuwa kungwi ana jukumu la kuwafundisha wanawari kuhusu masuala ya unyumba yakiwemo usafi wa mwili na nyumba, namna ya kumhudumia mume, namna ya kusema na marafiki na jamaa za mume, matumizi ya vifaa vya kiasili kama vile mbuzi, kinu, mchi ufagio miongoni mwa mengine. Aidha, maudhui haya ya ukungwi yanafundishwa na waimbaji wa nyimbo teule za taarab</p>2025-07-18T13:48:48+00:00##submission.copyrightStatement##https://journals.eanso.org/index.php/eajss/article/view/3382Athari ya Uhawilishaji wa Viwakilishi vya Jinsia kwa Ujumbe wa Lugha Chanzi; Tafsiri Kutoka Kiswahili Kwenda Kiingereza2025-07-24T19:33:27+00:00Mutisya Cosmas Mbithisamwelngetich001@gmail.comSarah Ndanu Ngesu, PhDcosmasmutisyam@gmail.comEsther N. Chomba, PhDcosmasmutisyam@gmail.com<p>Suala la athari katika uhawilishaji wa kwenye ujumbe wa lugha chanzi katika tafsiri si geni. Tafiti nyingi zimelishughulikia suala hili lakini tafiti hizo zimeegemea sana katika athari ya uhawilishaji wa ujumbe kutoka lugha ya Kiingereza kwenda Kiswahili. Lengo la utafiti huu lilikuwa kuchunguza athari ya uhawilishaji wa kwa ujumbe wa lugha chanzi katika tafsiri kutoka Kiswahili kwenda Kiingereza. Data za utafiti zilipatikana kwa kusoma, kuchanganua na kuhakiki tafsiri ya vitabu teule vya fasihi: <em>Siku Njema</em> ya Walibora (1996) na tafsiri yake <em>A Good Day</em> iliyotafsiriwa na Kweyu na Kawegere (2019), <em>Kaburi bila Msalaba</em> iliyoandikwa na Kareithi (1969) na tafsiri yake ya Kiingereza <em>Unmarked Grave</em> iliyotafsiriwa na Githiora (2019). Vilevile, mtafiti aliangazia tamthilia mbili; Tamthilia ya <em>Natala</em> iliyoandikwa na Mberia (1997) na tafsiri yake ya Kiingereza <em>Natala</em> iliyotafsiriwa na Kasu na Marami (2011). Tamthilia ya <em>Kinjekitile</em> iliyoandikwa na Hussein (1969) na tafsiri yake <em>Kinjekitile</em> iliyotafsiriwa na Hussein mwenyewe (1970) ilichunguzwa. Mtafiti aliteua vitabu hivi kwa kuwa vilionesha utajiri wa data inayohusu uhawilishaji wa jinsia. Utafiti huu uliongozwa na Nadharia ya <em>Skopos</em> na Nadharia ya Usawa wa Kidhima. Nadharia ya <em>Skopos</em> iliyoasisiwa na Hanns Vermeer (1989) ambayo husisitiza kuwa, kimsingi kutafsiri kunafaa kushughulikia jukumu la matini chanzi na matini lengwa yaani tafsiri ni kitendo chenye malengo. Nadharia ya Usawa wa Kidhima iliasisiwa na Nida (1964) na inatilia mkazo usawa wa kimaana na athari sawa kwa hadhira katika mchakato wa tafsiri. Natharia hizi zilisaidia kuchuguza athari ya uhawilishaji wa kwa ujumbe asilia katika vitabu teule. Data ya utafiti huu ilipatikana kwa kusoma na kuainisha katika vitabu teule vilivyotafsiriwa kutoka kiswahili kwenda kiingereza. Baada ya kubainisha uhawilishaji wa data hiyo ilichanganuliwa kitaamuli na kitakwimu na matokeo kuwasilishwa kupita maandishi ya kinadhari majedwali na michoro ya miche duara kutathimini athari ya uhawilishaji huo kwa ujumbe wa lugha chanzi. Matokeo ya utafiti huu yanaonesha kuwa wafasiri wa vitabu teule wamehawilisha na uhawilishaji huo ukawa na athari kwa ujumbe asilia. Uhawilishaji wa unachangamoto nyingi kwa hivyo wafasiri wanapaswa kumakinika kwani, uhawilishaji wa huwa na athari hasi na chanya kwa hadhira lengwa. Utafiti huu unapendekeza utafiti zaidi kufanywa katika uhawilishaji wa viwakilishi vya nyakati katika tafsiri kutoka Kiswahili kwenda Kiingereza kwani kama uhawilishaji wa , uhawilishaji wa viwakilishi vya wakati vilevile, vinaweza kuwa na athari kwa ujumbe asilia.</p>2025-07-24T00:00:00+00:00##submission.copyrightStatement##https://journals.eanso.org/index.php/eajss/article/view/3427Tathmini Ya Sura Za Ufisadi Katika Riwaya Za Tom Olali Mafamba (2012) Na Watu Wa Gehenna (2012)2025-08-04T22:34:29+00:00Pauline Musyokipaulina.musyoki1@gmail.comJessee Murithi, PhDpaulina.musyoki1@gmail.com<p>Utafiti huu unaeleza sura tofauti za ufisadi. Mtafiti amefanya hivi kwa kushughulikia riwaya ya Mafamba (Olali, 2012) na Watu Wa Gehenna (Olali, 2012). Ufisadi ni suala tata ulimwenguni na hata nchini Kenya. Dhana hii ni pana ila maelezo yake katika fasihi ni finyu kwa kuwa, msisitizo umekuwa kwenye usimamizi wa fedha za umma. Kulingana na Tume ya EACC (2016) kipengele cha IV, ufisadi unahusu unyanyasaji katika ofisi za umma, upendeleo, hongo, ulaghai, ukosefu wa uaminifu katika ofisi za umma, kutolipa ushuru au ada yoyote ile na kutofuata sheria zilizohidhinishwa kuteua viongozi katika ofisi za umma. Mtafiti ameangazia masuala hayo kwa kutathmini riwaya teule kwa lengo la kubainisha namna masuala hayo yalivyosawiriwa na kuleta uwezekano wa sura tofauti za ufisadi. Wahakiki kama vile; Muthumbi (2005) anaeleza ufisadi kama wizi wa pesa, Ochenga (2008) anaelezea ufisadi kama matumizi mabaya ya pesa za umma, Mayiek (2015) Ufisadi ni wizi wa mali ya umma, Sereti (2016) Ufisadi ni hali ya kujilimbikizia raslimali za taifa, Mwaniki (2018) Ufisadi ni unyakuzi wa mali ya umma.wahakiki hawa na wengineo wameeleza ufisadi kama matumizi mabaya ya fedha za umma na ndio sababu utafiti huu umeangazia sura tofauti za ufisadi. Riwaya zimeteuliwa kimakusudi na zimeangazia sura tofauti za ufisadi hivyo zilitupa data mwafaka. Nadharia ya Udenguzi ilitumika. Nadharia ya Udenguzi ilihusishwa na Jacques Derrida (1962).Waitifaki wake ni pamoja na Foocult, Roland Barthes, Jean Baudrillar, Paul Deman, J. Hills Miller, Jacques Lacan Barbara Johnstone na wengineo. Kupitia mihimili ya nadharia hii mtafiti alieleza fasiri mbalimbali za ufisadi. Utafiti huu ulifanywa maktabani kwa kusoma vitabu teule, tasnifu, majarida na makala ya mitandaoni yanayohusiana na mada. Data ya kimsingi ilitolewa kwenye riwaya teule. Data hiyo ilichanganuliwa kwa kuzingatia malengo na nadharia inayoongoza utafiti. Matokeo yamewasilishwa kwa kutumia njia ya maelezo. Utafiti huu utakuwa muhimu kwa wasomi na jamii kwa jumla hasa kwa kuagazia suala tata la ufisadi.</p>2025-08-04T22:33:43+00:00##submission.copyrightStatement##https://journals.eanso.org/index.php/eajss/article/view/3469Mikakati ya Ushawishi katika Manifesto ya Kenya Kwanza katika Uchaguzi Mkuu wa 2022 Nchini Kenya2025-08-11T22:06:34+00:00Nancy Chepkemoi Koneskonesnancy2013@gmail.comRaphael Mwaura Gacheiyakonesnancy2013@gmail.com<p>Utafiti huu ulishughulikia mikakati ya ushawishi katika manifesto ya Muungano wa Kenya Kwanza katika uchaguzi mkuu wa 2022 nchini Kenya. Ulichunguza iwapo mikakati hiyo ilichangia katika kujenga mvuto wa kisiasa na uungwaji mkono katika uchaguzi mkuu wa Kenya. Lengo mahususi la utafiti huu lilikuwa kuchunguza jinsi mikakati ya ushawishi ilisawirika katika manifesto. Utafiti uliongozwa na Nadharia ya Uchanganuzi Hakiki wa Usemi kuchanganua namna lugha inavyotumika kisiasa. Utafiti ulikuwa wa kithamano na ulitekelezwa kwa kutumia mbinu ya kifasili. Sampuli teule ya kimakusudi ilihusisha manifesto ya Kenya Kwanza. Deta ilikusanywa kutoka kwenye tovuti ya Muungano wa Kenya Kwanza. Ilichanganuliwa kwa kuangalia maudhui ya lugha ya ushawishi. Matokeo yalionesha kuwa lugha katika manifesto ililenga kuibua matumaini na ahadi ya maisha bora kwa wananchi. Makala hii inachangia maarifa katika taaluma ya Isimu, hasa katika muktadha wa kisiasa. Pia, inawapa wagombezi wa siasa mwongozo wa kuunda manifesto zenye mvuto, na inasaidia mashirika ya utafiti wa kisiasa kubuni sera na miongozo bora ya uchaguzi</p>2025-08-11T19:48:50+00:00##submission.copyrightStatement##https://journals.eanso.org/index.php/eajss/article/view/3485-2025-08-13T20:23:40+00:00Mukonambi Kekonen Stanleystanleymukonambi@gmail.comTitus Kaui, PhDkauititus@ku.ac.ke<p>Makala hii inachunguza ubainishaji wa wakaa katika hotuba teule za wanasiasa wa Kenya. Baadhi ya wanasiasa hutoa hotuba zinazovuta makini ya wasikilizaji na wafuasi wao kwa mitindo tofauti. Mojawapo wa mbinu hii ya kimtindo ni usimulizi. Wakaa ni mojawapo wa kipengele cha kimtindo katika usimulizi. Tafiti kadha zimefanywa kubainisha wakaa na matumizi yake katika tanzu za fasihi andishi na fasihi simulizi (taz. Kwaka; 2015; Khamis; 2015; Muiya; 2018; Kinga; 2020; Asige, 2021). Licha ya hayo, tafiti hizi za awali hazikushughulikia wakaa kwa kuhusisha moja kwa moja si hotuba tu bali hotuba za kisiasa. Ni katika msingi huu ndipo makala hii imechunguza jinsi wakaa inavyojitokeza katika hotuba teule za wanasiasa wa Kenya. Makala hii imeelekezwa na nadharia ya Naratolojia iliyoasisiwa na mwanafalsafa Plato katika chapisho lake <em>The Republic</em> na baadaye ikaendelezwa na mwanafunzi wake Aristotle (1920) aliyewasilisha mawazo yake katika chapisho la <em>The Poetics</em> na wananaratolojia wa hivi majuzi Gennette (1980), Prince (1982) na Rimmon-Kenan (2002). Uchunguzi huu ulizingatia mawazo yake Rimmon-Kenan. Naratolojia ni stadi ya aina ya utendaji kazi wa usimulizi. Huangalia undani wa vifaa vinavyoongoza maelezo ya simulizi na ufahamu wa utendaji kazi wake. Data iliyotumika katika makala hii imetokana na kusoma machapisho maktabani kama vile tasnifu, majarida na vitabu. Halikadhalika, utazamaji, usikilizaji na uchambuzi wa hotuba teule za wanasiasa Mhes. Kenyatta, Odinga na Ruto katika mtandao wa <em>YouTube</em> ulihusishwa. Matokeo ya utafiti yamedhihirisha kuwepo kwa vipengele vya wakaa vya mpangilio, muda na idadi au umara katika hotuba za wanasiasa. Isitoshe, imebainika kuwa kipengele hiki cha usimulizi kimetumiwa kuendeleza maudhui, fani za lugha na kuchimuza wahusika</p>2025-08-13T20:22:23+00:00##submission.copyrightStatement##https://journals.eanso.org/index.php/eajss/article/view/3510Mtindo na Matumizi ya Lugha Katika Muziki wa Taarab : Mifano Kutoka Taarab za Kiswahili2025-08-19T08:49:29+00:00Felix Kwame Sosoofksosoo@ug.edu.gh<p>Makala hii inajadili juu ya mtindo na matumizi ya lugha katika Muziki wa Taarab kwa kutumia mifano kutoka Taarab za Kiswahili. Kwa kutumia nadharia ya umuundo makala hii inaibua vipengele vya lugha vinavyotumika katika Taarabu, kuelezea dhima ya uteuzi wa vipengele vya lugha na kujadili dhamira zinazoibuka kutokana na matumizi ya vipengele vya lugha katika Taarab. Katika kufikia lengo hilo makala hii inajibu maswali yafuatayo; Je, ni vipengele vipi vya lugha vinavyojichomoza zaidi katika Taarab? Je ni kwa nini wasanii huamua kuteua kutumia vipengele hivyo vya lugha? Na, ni dhamira zipi zinazoibuka kutokana na matumizi ya vipengele hivyo vya lugha?</p>2025-08-19T08:48:29+00:00##submission.copyrightStatement##https://journals.eanso.org/index.php/eajss/article/view/3527Athari za Ubadilishaji Msimbo Kanisani kwa Wasikilizaji: Mifano Kutoka katika Mahubiri ya Mchungaji Wilbroad Mastai2025-08-21T14:46:13+00:00Amulike Abraham Mwampambaamulikemwampamba@gmail.com<p>Utafiti huu ulihusu athari za ubadilishaji msimbo kanisani kwa kuchunguza mahubiri ya Mchungaji Wilbroad Mastai. Lengo la utafiti lilikuwa kubainisha athari za ubadilishaji msimbo kwa wasikilizaji wa mahubiri ya Mchungaji Wilbroad Mastai. Data za utafiti huu zilikusanywa kwa njia ya hojaji katika Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania, kata ya Kimara, Manispaa ya Ubungo jijini Dar es salaam. Kadhalika utafiti huu uliongozwa na Nadharia ya Maki ya Carol Myers-Scotton (1993). Utafiti ulitumia usampulishaji nasibu tabakishi kuwapata watoa taarifa hamsini (50). Matokeo ya utafiti yalionesha kuwa wasikilizaji wanapata athari chanya (41.2%) na hasi (58.8%) kutokana na ubadilishaji msimbo katika mahubiri ya Mchungaji Wilbroad Mastai. Kwa hiyo, kutokana na matokeo ya utafiti huu ni wazi kwamba ubadilishaji msimbo katika mahubiri ni jambo lisilokubalika kwa wengi. Hii ni kutokana na athari hasi kuwa katika kiwango cha juu ukilinganisha na athari chanya. Aidha, utafiti huu ulipendekeza kwamba tafiti zingine zifanyike kuhusu sababu za ubadilishaji msimbo katika mahubiri ya Mchungaji Wilbroad Mastai pamoja na kuchunguza athari za ubadilishaji msimbo katika dini zingine</p>2025-08-21T14:02:24+00:00##submission.copyrightStatement##https://journals.eanso.org/index.php/eajss/article/view/3531Mtazamo Linganishi wa Itikadi katika Utenzi wa Mwanakupona na Mashairi ya Muyaka2025-08-21T14:46:13+00:00Doreen Nkathankathadoreen13@gmail.comJessee Murithi, PhDmurithijj2015@gmail.com<p>Makala hii imechunguza itikadi katika <em>Utenzi wa Mwanakupona</em> na mashairi ya Muyaka. Itikadi ni mawazo ambayo hujumuisha malengo, matamanio na matarajio, na matendo ya mtu. Dhana ya itikadi pia imefasiriwa kama matamanio, fikra, malengo na maelezo ya mtunzi kuhusu masuala ya kijamii ya kisiasa, kidini, na kiuchumi kwa ujumla wake. Hivyo, itikadi kama imani ambazo huelekeza matendo ya binadamu yeyote ulimwenguni zimewaathiri watunzi wa kazi hizi mbili kwa namna wanavyosawiri mitazamo yao kuhusu wanavyowasilisha. Huelekeza matendo yale mtunzi atakayowasilisha na namna atakavyowasilisha kazi yake. <em>Utenzi wa Mwanakupona </em>na mashairi ya Muyaka ni kazi zilizoandikwa katika kipindi kimoja lakini utofauti unajitokeza wa kimtindo. Kwa hivyo, ni muhimu kuchunguza na kuzilinganisha itikadi zilizowaongoza watunzi hawa. Nadharia ya itikadi; mikabala ya Karl Marx (1977), Louis Althusser (1981) na Antonio Gramsci (1985), ilitumika. Mkabala wa Karl Marx ulitumiwa sababu dhana ya "ung’amuzi potoshi," mkabala wa Althusser ulitumiwa kwani unaorodhesha vyombo vya kiitikadi na mkabala wa Gramsci ulitumiwa sababu ya dhana ya ukubalifu na ukawaida. Data ya makala hii ilikusanywa maktabani. Vitabu teule, majarida na makala kuhusu mada husika mtandaoni yalisomwa kwa kina na kuchambuliwa. Mbinu ya usampulishaji wa kimaksudi ilitumika katika uteuzi wa sampuli. Kutokana na data ya utafiti huu, imebainika kuwa itikadi zinazowaongoza Muyaka na <em>Mwanakupona</em> ni tofauti kwani wanasawiri kazi yao kwa namna tofauti ingawa walikuwa watunzi wa kipindi cha kirasimi. Muyaka ilibainika kuwa aliongozwa na itikadi ya mapinduzi ya nguvu, uhuru wa kiakili na ukandamizaji. <em>Mwanakupona</em> kwa upande mwingine imebainika ameongozwa na itikadi ya utiifu, ukubalifu na ukawaida na hata ubabedume. Makala hii inapendekeza kuwa tafiti zingine zaidi kuhusu itikadi zinaweza kufanywa kuhusu tenzi za mwanzoni na kuzilinganisha, mikabala mingine za itikadi pia inaweza kutumika na pia utafiti zaidi unaweza kufanywa kuhusu utenzi wa <em>Mwanakupona</em> kuhusu wanatapo wa tatu.</p>2025-08-21T14:28:43+00:00##submission.copyrightStatement##https://journals.eanso.org/index.php/eajss/article/view/3542Mtagusano wa Kimofofonolojia katika Kiolezofaridi cha Lugha ya Kiswahili: Mapengo ya Kiolezofaridi2025-08-25T18:01:57+00:00Naomi Ndumba Kimonyenaomikimonye33@gmail.comLeonard Chacha Mwitachachamwita8@gmail.comPeter Githinjipeter.githinji@ku.ac.ke<p>Makala hii inalenga kubainisha mapengo kwenye violezofaridi vya kimofofonolojia katika lugha ya Kiswahili. Kiolezofaridi ni mfumo wa mpangilio wa vipengee vya kiisimu ambao unaonyesha uhusiano wima baina ya kipashio kimoja na vipashio vingine katika muktadha maalum, yaani ni mfumo wa miundo ya kisarufi. Pengo la kimofofonolojia hutokea pale ambapo kipashio fulani cha lugha kinakubalika licha ya kuwa kimekiuka sheria za uundaji na mnyambuliko wa maneno. Pia hutokea pale ambapo hata baada ya kuzingatia sheria hizi tunapata kipashio ambacho hakikubaliki katika lugha. Katika utafiti huu, kuna maumbo yanayotii kanuni za kisarufi lakini hayakubaliki kiisimu ilhali kuna yale ambayo yamekaidi kaida za kisarufi lakini yanakubalika. Katika mofolojia, kanuni za kimofolojia zinapokiukwa katika uambishaji, tunatarajia kuwa maumbo yatakayozalishwa yatakuwa na makosa ya kisarufi na hivyo kutotumika. Kwa upande mwingine, maumbo ya lugha yanapokubalika licha ya kutozingatia kanuni za kimofolojia ni ishara kuwa kuna pengo la kiolezofaridi katika kiwango cha kimofolojia. Mofolojia hutagusana sana na michakato ya kifonolojia; hivyo basi katika makala hii tutashuhudia jinsi fonolojia inavyoathiri kiolezofaridi cha kimofolojia. Nadharia ya Kiolezofaridi Bora (Optimal Paradigms) iliyoasisiwa na McCarthy (2005) ndiyo iliyotumika. Misingi ya nadharia hii ni; kwanza, mshindani huzingatia vielelezo vya unyambuaji pale ambapo kiolezo cha unyambuaji huwa na maneno yaliyojikita kwenye msamiati mmoja. Pili, mashartizuizi ya uadilifu na uziada hutathmini washindani. Ukiukaji wa mashartizuizi wa kila kipashio hujumuishwa. Tatu, maumbotokeo hufanana na vielelezo vya vipashio vingine na hatimaye kuna makundi ya maumbotokeo ya mashartizuizi ya uadilifu yanayofanana. Data ya utafiti huu ilikusanywa maktabani na mtandaoni. Watafiti walisoma kwa kina vitabu vya lugha ya Kiswahili ambavyo vimechapishwa, tasnifu za lugha na pia, makala zilizochapishwa mtandaoni ili kupata data iliyohitajika. Asili ya data ni matini teule za isimu na data yenyewe ni violezofaridi vyenye mapengo. Usampulishaji dhamirifu ulitumika kuteua kazi za isimu. Data iliteuliwa kimakusudi na kuwasilishwa kwa njia ya maelezo na majedwali. Matokeo ya utafiti huu yaliweka wazi kuwa mapengo katika lugha ya Kiswahili husababishwa na hali mbalimbali. Utafiti huu umebainisha kuwa katika lugha Kiswahili, mapengo ya violezofaridi yapo kwenye matawi ya fonolojia, mofolojia, sintaksia na semantiki.</p>2025-08-25T15:42:32+00:00##submission.copyrightStatement##https://journals.eanso.org/index.php/eajss/article/view/3544Mchango wa Ukafsiri katika Kukuza Isimu-Kokotozi: Mfano wa Nyimbo za Injili za Ambassadors of Christ na The Saints Ministers2025-08-25T20:52:56+00:00Ayub Oyimba Barasaayubbarasa86@gmail.comJohn Kirimi M’raijijmraiji@mmust.ac.keFred Simiyu WanjalaWsimiyu@kibu.ac.ke<p>Ukafsiri ni taaluma muhimu katika tasnia ya isimu kokotozi ya Kiswahili na katika ufanikishaji wa mawasiliano. Aidha, taaluma ya ukafsiri inayohusu uhawilishaji wa ujumbe ama wa matini andishi kwenda mazungumzo. Au kutoka mazungumzo na kwenda katika maandishi. Imetekeleza jukumu hili la mawasiliano kwa njia ya kipekee kupitia Tehama. Katika karne hii ya 21, ukafsiri umetumia Teknolojia habari na mawasiliano (kuanzia sasa, Tehama) kama jukwaa la kutekeleza mawasiliano kwa umma mpana na kwa wakati mfupi iwezekanavyo. Aidha, lugha mbalimbali zimekuwa zikitumika na hata kutafsiriwa na zingine kukalimaniwa kwa lugha lengwa kwa minajili ya kufanikisha mawasiliano. Hii inaonesha kuwa kumekuwa na mshawasha wa kutaka kufikia idadi kubwa ya hadhira inayojua kusoma na isiyojua kusoma kwa lugha wanazozielewa. Makala hii inaongozwa na nadharia ya Ulinganifu Amilifu na ya Mawasiliano kutathmini nafasi ya Tehama katika kukuza na kuendeleza Kiswahili hasa katika Ukanda wa Afrika Mashariki huku ikijikita katika ukafsiri wa nyimbo za Ambassadors of Christ na The Saints Ministers zilizokafsiriwa kutoka Kiswahili hadi Kiingereza. Utafiti huu ulifamywa Maktabani. Upekuzi Wa vyanzo vya Utafiti pamoja na vitabu, kusikiza Kanda za video, tasnifu na wavuti na Kisha kuwasilisha kwa maelezo ya kinathari. Tehama ilisaidia kuondoa utata wa ulinganifu wa maana katika Matini chanzi kwenda Matini lengwa kwa kuambatanisha picha, kutumia fonti Tofautitofauti, alama za uakifishaji kama vile hisi, maswali ya balagha, lugha ishara na hata miondoko ya waimbaji ili kusaidia kukuza uelewa wa hadhira pokezi. Inatarajiwa kwamba utafiti utaongeza maarifa ya ukafsiri, usomaji na uhakiki wa kazi zilizokafsiriwa na kuwafaidi Wanafunzi, Wakafsiri, Walimu na Watafiti wa baadaye</p>2025-08-25T00:00:00+00:00##submission.copyrightStatement##https://journals.eanso.org/index.php/eajss/article/view/3559Falsafa ya Umoja na Mshikamano katika Misemo ya Vyombo vya Usafiri katika Ziwa Tanganyika2025-08-27T22:07:10+00:00Anna Ussiryannaussiry87@gmail.comMohamed Maguoomarymohamed36@gmail.comSalma Hamadsalma.hamad@out.ac.tz<p>Makala haya yanaangazia falsafa ya umoja na mshikamano katika misemo ya vyombo vya usafiri katika ziwa Tanganyika ikiwa ni moja kati ya vipengele vya falsafa ya Kiafrika. Lengo la makala haya ilikuwa ni kutaka kuona namna falsafa ya Kiafrika kupitia kipengele cha umoja na mshikamano inavyojitokeza na kuwasilishwa katika misemo hiyo. Uandishi wa makala uliongozwa na nadharia ya Sosholojia ya Fasihi ambapo suala la falsafa ni sehemu ya jamii na hivyo nadharia hii ni faafu. Data ya makala hii ilikusanywa kwa kutumia mbinu ya usomaji makini na kuchambuliwa kwa kutumia mbinu ya kimaelezo. Makala imebainisha kwamba falsafa ya umoja na mshikamano inajitokeza katika misemo ya vyombo vya usafiri wa majini katika ziwa Tanganyika kupitia misemo ambapo ni umoja na mshikamano ni kupendana, umoja na mshikamano ni kuepuka chuki, umoja na mshikamano ni kuwajali wageni, umoja na mshikamano ni kusaidiana, umoja na mshikamano ni kubarikiwa, umoja na mshikamano ni kuelimishana na umoja na mshikamano katika kuonyana. Makala yanatoa mapendekezo kwamba utafiti kama huu ufanyike kwa kutazama falsafa ya misemo ya kwenye vyombo vya usafiri wa majini katika maziwa na mito mingine ya jamii mbalimbali ili kuweza kupata picha kamili ya falsafa ya umoja na mshikamano katika jamii</p>2025-08-27T22:06:28+00:00##submission.copyrightStatement##https://journals.eanso.org/index.php/eajss/article/view/3591Mkakati Wa Uhalalishaji wa Kimamlaka katika Hotuba Teule za Marais wa Tanzania katika Vikao vya Pamoja vya Mabunge ya Kitaifa, Kenya2025-09-05T10:54:11+00:00Sammy Dimbudimbuliana@gmail.comJohn Kobia, PhDdimbuliana@gmail.comMary Kanyua, PhDdimbuliana@gmail.com<p>Makala hii ilihusu uhalalishaji wa kimamlaka katika hotuba teule za Marais wa Tanzania katika vikao vya pamoja vya Mabunge ya Kitaifa nchini Kenya. Nadharia iliyoongoza makala hii ni Uchanganuzi Makinifu wa diskosi. Nadharia hii hudokeza kuwa lugha kivyake haina mamlaka, bali huyapata itumiwapo na wenye mamlaka katika miundo ya kijamii. Sampuli ya makala hii ilipakuliwa kutoka kumbukumbu za kudumu za Mabunge ya Kitaifa nchini Kenya zilizoko mtandaoni. Diskosi za hotuba teule za Marais Jakaya Kikwete na Samia Suluhu zilizo sampuli ya makala hii ni zile zilizowasilishwa kati ya miaka (2013-2022). Kipindi hiki ni awamu ya 11 na awamu ya pili na tatu ya Mabunge ya Kitaifa na Seneti nchini Kenya. Jumla ya hotuba mbili ziliteuliwa kimakusudi kwa kujikita kwenye mbinu ya uchanganuzi wa yaliyomo. Kifaa cha utafiti kilichotumika katika ukusanyaji wa data ni orodha ya ukaguzi. Muundo wa kimaelezo ulitumika katika kukusanya, kuchambua na kuwasilisha matokeo ya makala. Data ya makala hii ilikusanywa kutokana na mchakato wa usomaji wa kina wa hotuba teule. Matokeo ya makala hii yalidhihirisha kuwa mikakati ya kibinafsi, wataalamu, mfano wa kuigwa, yasiyo binafsi, upatanishi wa kimila. Makala hii ilipendekeza kuwa utafiti wa baadaye ufanywe kuhusu namna vipengele vya mkakati wa uhalalishaji wa mamlaka hutambulisha wahutubu katika hotuba za kisiasa</p>2025-09-05T10:49:48+00:00##submission.copyrightStatement##https://journals.eanso.org/index.php/eajss/article/view/3587Mahusiano ya Uwezo katika Muwala wa Mada katika Hotuba Teule za Marais Kikwete na Samia, Kenya2025-09-05T10:54:11+00:00Sammy Dimbudimbuliana@gmail.comJohn Kobia, PhDdimbuliana@gmail.comMary Kanyua, PhDdimbuliana@gmail.com<p>Muwala huchukuliwa kuwa kipengele cha diskosi ambacho hufasiriwa kulingana na muktadha na hujumuisha dhana zinazohusiana, utathmini na msemezano. Makala hii iliangazia makala muwala wa mada katika hotuba teule za Marais Jakaya Kikwete (Kikwete) na Samia Suluhu (Samia). Nadharia iliyoongoza makala hii ni Uchanganuzi Makinifu wa Diskosi. Nadharia hii hudokeza kuwa lugha yenyewe haina mamlaka bali huyapata inapotumiwa na wenye mamlaka katika miundo ya kijamii. Sampuli ya makala hii ilipakuliwa kutoka Kumbukumbu za Kudumu za Mabunge ya Kitaifa nchini Kenya zilizoko mtandaoni. Diskosi za hotuba teule zilizo sampuli ya makala hii ni zile zilizowasilishwa kwa lugha ya Kiswahili baina ya miaka (2013-2022). Kipindi hiki ni awamu ya 11 na 12 ya Bunge la Kitaifa na awamu ya 2 na 3 ya Bunge la Seneti nchini Kenya. Jumla ya hotuba 2 ziliteuliwa kimakusudi kwa kujikita kwenye mbinu ya uchanganuzi wa yaliyomo. Muundo wa kimaelezo ulitumika katika kukusanya, kuchambua na kuwasilisha matokeo ya utafiti. Data ya makala hii ilikusanywa kutokana na mchakato wa usomaji wa kina wa hotuba teule. Data iliainishwa kulingana na maswali ya utafiti. Matokeo yalibainisha kuwa vipengele vya kigezo cha hali, washiriki katika diskosi, madhumuni ya mawasiliano, kitendo neni kilichotendwa na kaida za mawasiliano yalikuza muwala wa mada katika hotuba teule. Makala hii ilibainisha namna masuala ya kimuktadha huchangia muwala wa ndani na wa kijumla ili kuleta uelewaji wa diskosi ili kukuza mahusiano ya uwezo katika diskosi. Makala hii ilipendekeza tafiti za baadae zifanywe kuhusu namna vibainishi vya muktadha wa diskosi hukuza maana ya implikecha.</p>2025-09-05T10:50:05+00:00##submission.copyrightStatement##https://journals.eanso.org/index.php/eajss/article/view/3610Mtazamo wa Wanafunzi wa Kiswahili kama Lugha ya Kigeni kuhusu Hofu ya Kuitumia ChatGPT kama Zana ya Kujifunzia Kiswahili2025-09-10T13:28:49+00:00Sephania Mungasyeghe Kyungusephaniakyungu06@gmail.comFilipo Gao Lubua, PhDfilathemr@yahoo.comElither Vincent Kindole, PhDkindoleelither@yahoo.com<p>Makala hii imechunguza mtazamo wa wanafunzi wa Kiswahili kama lugha ya kigeni (kuanzia sasa, LgK) kuhusu hofu ya kuitumia ChatGPT kama zana ya kujifunzia Kiswahili. Lengo la makala hii lilikuwa kuibua maarifa kuhusu hofu inayowakumba wanafunzi wanaoitumia ChatGPT kama zana ya kujifunzia Kiswahili. Kwa sababu tafiti nyingi zilizochunguza mtazamo wa wanafunzi wa LgK wanaoitumia ChatGPT zimejikita zaidi kwa wanafunzi wanaojifunza Kiingereza kama LgK. Aidha, tafiti hizo zinaonesha kuwa ingawa wanafunzi wengi wa Kiingereza kama LgK wana mtazamo chanya kuhusu matumizi ya ChatGPT kama zana ya kujifunzia Kiingereza, wapo wengine hukumbwa na hofu wanapoitumia zana hiyo. Data za utafiti huu zilikusanywa kutoka kwa wanafunzi wanaojifunza Kiswahili kama LgK katika vituo viwili vinavyofundisha Kiswahili kwa wageni nchini Tanzania ambavyo ni TATAKI na MS TCDC. Sampuli ya utafiti huu ilikuwa ni wanafunzi 10 kutoka katika vituo teule ambayo ilipatikana kwa mbinu ya usampulishaji lengwa na fursa. Data kutoka katika sampuli hiyo zilikusanywa kwa mbinu ya usaili na kuwasilishwa kitaamuli, na kuchambuliwa kwa kuongozwa na Modeli ya Ukubalifu wa Teknolojia. Matokeo ya utafiti huu yanaonesha kwamba wanafunzi wa Kiswahili kama LgK wanaoitumia ChatGPT kama zana ya kujifunzia Kiswahili wanakumbwa na hofu ya kuitegemea ChatGPT kupita kiasi, majibu yasiyo sahihi yanayotolewa na ChatGPT, Kiswahili kinachotumiwa na ChatGPT, kutoamini kama ChatGPT inaelewa wanachotaka, na hofu ya ChatGPT kuwa ya kulipia. Utafiti huu unapendekeza elimu itolewe kwa wanafunzi wa Kiswahili kama LgK namna sahihi ya kuitumia ChatGPT kwani hofu zingine zimebainika kuwa zinatokana na ukosefu wa maarifa ya jinsi ya kuitumia</p>2025-09-10T12:53:56+00:00##submission.copyrightStatement##https://journals.eanso.org/index.php/eajss/article/view/3629Leksia katika Diskosi za Wabunge Wanawake kutoka Bunge la Taifa Zinazojenga Utambulisho Kuhusiana na Mamlaka2025-09-12T17:11:51+00:00Nkanga Mishecknkangamisheck@gmail.comMwembu Kimathi, PhDkwamwembu@gmail.comMicheni Mutegidmisheni@gmail.com<p>Diskosi za kisiasa hufanya kazi kubwa katika kujenga na kuidhinisha utambulisho wa mwanasiasa, utambulisho wa kikundi chake na uanachama wake. Kupitia lugha, wanasiasa utambulisho wa mwanasiasa na ushirika wao kwa kikundi unaweza kugunduliwa kupitia upeaji wa kiutambulisho. Peo ya utambulisho hukuza imani na ukubalifu wa mzungumzaji kwa wasikilizaji wake. Upeaji wa utambulisho, hutegemea uteuzi na utumiaji wa leksia maalumu. Utafiti huu umechunguza upeaji wa kiutambulisho katika diskosi za wabunge wanawake kutoka Bunge la Taifa nchini Kenya. Lengo la utafiti huu lilikuwa kuchunguza leksia zilizotumika katika upeaji wa utambulisho kwenye diskosi za wabunge wanawake. Utafiti huu uliongozwa na nadharia ya Uchanganuzi wa Peo na mtazamo wa Uchanganuzi Hakiki-Makinifu wa Usemi. Nadharia hizi zilitumika kutathmini namna leksia zilizotumika kujenga utambulisho wa jinsia kuhusiana na mamlaka. Chanzo cha data katika utafiti huu; ni video kutoka mtandao wa YouTube ambazo zilikuwa na hotuba zilizowasilishwa kwa umma na wabunge wanawake 169, waliochaguliwa na wananchi katika bunge la 11, 12 na 13 la taifa la Kenya, zilihifadhiwa. Wasailiwa hao ni wanawake 111 wanaowakilisha kaunti pamoja na wanawake 58 waliochaguliwa kuwakilisha maeneobunge mbalimbali katika Bunge la Taifa. Mbinu ya utafiti iliyotumika kukusanywa data ilikuwa utazamaji na usikilizaji wa sauti ninga kutoka kwa mtandao ya YouTube. Utafiti huu umebaini kuwa, matumizi ya kiisimu ya leksia kwenye diskosi za wabunge wanawake hujenga utambulisho kuhusiana na mamlaka, kuambatana mamahitaji ya kibinafsi na kikundi. Leksia katika diskosi za wabunge wanawake, zilitambulisha wanawake katika kiwango cha kibinafsi, kieneo na kimakundi. Kwa hivyo, upeaji wa utambulisho ulidhihirisha migao wa kibinafsi, kimaeneo, kimahusiano, kiutendaji na kimakundi katika ujenzi wa utambulisho wa wanawake.</p>2025-09-12T17:09:22+00:00##submission.copyrightStatement##https://journals.eanso.org/index.php/eajss/article/view/3653Miundo Taswira katika Sitiari za Viungo vya Mwili: Mfano wa Methali za Kiswahili2025-09-16T18:20:10+00:00Murule Otipa Remmyalexmwita44@gmail.comAkaka Linaremimuruch@gmail.comMavisi Roseremimuruch@gmail.com<p>Makala hii ilichunguza nafasi ya miundo taswira katika kuunda sitiari zinazopatikana katika methali. Utafiti huu ukiwa umekitwa katika sitiari tambuzi unalenga kuchunguza vile tajriba zilizomwiliwishwa kama vile uwiano na mwendo zinavyoakisiwa katika mahusiano ya kiistiari yaliyomo katika methali za Kiswahili. Methali ni hazina kuu ya hekima ya utamaduni na hutegemea sitiari kupitisha dhana za kidhahania za kijamii, kimadili au kihisia. Uchunguzi huu unahoji kuwa sitiari hizi si nasibu ila huundwa kiutaratibu kwa miundo taswira inayotokana na tajriba za kimwili. Miundo taswira ina nafasi muhimu katika kuunda maana za methali hususan zinazotumia sitiari za viungo vya mwili. Miundo taswira huunda miundo ya kimsingi ambayo sitiari hujengeka, haswa sitiari tambuzi ambapo dhana moja hueleweka kwa kuihusisha na nyingine. Sitiari za viungo vya mwili hutegemea uzoefu alio nao binadamu na mwili wake. Miundo taswira husaidia kuunganisha tajriba za mwili kwa maadili ya kidhahania kama vile mamlaka, werevu, maadili au tabia ya jamii. Uandishi wa makala hii uliongozwa na nadharia ya muundo taswira kwa mujibu wa Lakoff na Johnson (1980). Mkabala wa utafiti ni wa kithamano, muundo wa kimaelezo. Eneo la utafiti ni kamusi ya methali za Kiswahili. Kundi lengwa la utafiti ni methali za Kiswahili. Sampuli ya methali 10 zenye sitiari za viungo vya mwili ziliteuliwa kimaksudi kutoka katika Kamusi ya Methali za Kiswahili ya King’ei na Ndalu (2008) ili kuchunguzwa. Data ilikusanywa kwa usomaji makini wa methali zilizomo katika kamusi teule ya utafiti. Mtafiti akanakili methali hizo na miundo taswira iliyomo ikachunguzwa. Matokeo ya utafiti yalibainisha kuwa dhana zisizoshikika hueleweka kupitia kwa sitiari za viungo vya mwili kwa sababu ya mitagusano iliyopo baina ya binadamu na mazingira yake. Isitoshe utafiti umeipanua pia taaluma ya isimu ya Kiafrika kwa kuziweka diskosi za methali za Kiswahili ndani ya muktadha wa kiakili mbali na kuchangia katika nadharia ya sitiari za lugha tofauti, semiotiki ya kitamaduni na uhusiano baina ya lugha, fikra na jamii.</p>2025-09-16T17:39:54+00:00##submission.copyrightStatement##https://journals.eanso.org/index.php/eajss/article/view/3656Uchanganuzi wa Sauti ya Usimuliaji na Mahusiano ya Wakati wa Usimulizi katika Nyimbo Teule za Bahati Bukuku2025-09-17T10:41:37+00:00Asige Nelson Abogenaasige@gmail.com<p>Makala hii inalenga kubainisha jinsi sauti ya usimuliaji, kama kipengele muhimu cha kuhakiki simulizi, imejitokeza katika nyimbo teule zenye sifa za kisimulizi zilizowasilishwa na msanii Bahati Bukuku. Makala vilevile imechanganua mahusiano ya wakati wa usimulizi kwa kuhakiki vipengele vyake muhimu kama usimulizi baadaye, usimulizi kabla, usimulizi sawia na usimulizi zongomezi. Makala hii iliongozwa na lengo kuu la kudhihirisha jinsi vipengele vya sauti ya usimuliaji na mahusiano ya wakati wa usimulizi vinavyobainika katika nyimbo teule za Bahati Bukuku. Nyimbo zilizochanganuliwa ni: Lazima usamehe, Dunia haina huruma, Waraka, Tupatupa, Maamuzi, Ahabu, Unatisha. Vigezo vikuu vya uteuzi wa nyimbo hizi ni vipengele vya kihadithi ndani mwao. Nadharia iliyotumika ni ya Naratolojia inayojumuisha usimulizi katika tanzu za fasihi kama vile nyimbo, mashairi, maghani na kadhalika. Sauti ya usimulizi hujenga uhusiano na anayesimuliwa. Mtazamo wa masimulizi, mfuatano wa matukio pamoja na dhamira kuu huwasilishwa na msimulizi. Matukio katika simulizi hutendeka kiwakati. Simulizi hutambulishwa katika wakati fulani kuhusiana na kitendo cha usimuliaji: kabla ya kutendeka, wakati yanapotendeka, baada ya kutendeka na iwapo kuna uchangamano wa matukio kusimuliwa yakitendeka. Kwa mujibu wa matokeo, makala imebainisha kuwa mihimili ya sauti ya usimuliaji pamoja na mahusiano ya wakati wa usimuliaji ilijitokeza kwa namna mbalimbali katika nyimbo za msanii Bahati Bukuku kwa kutegemea miktadha mbalimbali. Makala ilihitimisha kuwa kigezo cha wakati ni nguzo muhimu katika uwasilishaji wa hadithi, na uelewa wa hadithi hutokana na matumizi sawa ya kigezo hiki, kwani matukio yanayosimuliwa hutendeka kiwakati.</p>2025-09-17T10:39:00+00:00##submission.copyrightStatement##https://journals.eanso.org/index.php/eajss/article/view/3674Kudhihirisha Namna Mwanamke Anavyoweza Kukabiliana na Athari Zinazotokana na Matumizi Hayo ya Lugha2025-09-18T14:51:20+00:00Mercy Kathambi MbaabuMercymbaabu@students.ku.ac.keEdwin Masinde, PhDemasinde254@gmail.com<p>Katika jamii nyingi za Kiafrika, lugha imekuwa chombo muhimu kinachotumika kuimarisha, kudumisha, au hata kupinga mitazamo ya kijinsia. Katika muktadha wa jamii ya Wameru, matumizi ya lugha yamekuwa yakielekeza mitazamo hasi dhidi ya wanawake katika uongozi, kwa njia ya kejeli, unyanyapaa wa kifasihi, na taswira dhalili zinazojengwa kupitia vyombo vya habari, mitandao ya kijamii, na mazungumzo ya kawaida. Utafiti huu unalenga kudhihirisha namna wanawake wanavyoweza kukabiliana na athari zinazotokana na matumizi hayo ya lugha, kwa kutumia Nadharia ya Uchunguzi tahakiki wa matini kama muktadha wa kimaandishi na kimaudhui.Kupitia uchambuzi wa matini kutoka majukwaa ya kijamii, hotuba za kisiasa, na mahojiano katika vyombo vya habari, utafiti huu umetambua kuwa lugha si chombo cha kieneo tu, bali ni uwanja wa mapambano wa kijamii. Mwanamke kiongozi, anapowekwa kwenye mizani ya lugha dhalishi, hujikuta akikabiliana na mashambulizi yasiyo ya moja kwa moja, bali yaliyojificha katika istilahi, tamathali na semi zinazobeba mizigo ya kiitikadi. Kwa kutumia misingi ya uchunguzi tahakiki matini kama ilivyowekwa na Fairclough (1995), utafiti huu umeangazia njia ambazo wanawake hutumia kuandika upya simulizi zao, kujenga utambulisho mbadala, na kutumia lugha yenye msimamo kuhimiza uaminifu wao wa kiuongozi. Wanawake hawa hujihami kwa kutumia hoja zenye msingi wa kitaaluma, kutekeleza majukumu yao kwa umakinifu, na kupinga kwa ufasaha taswira hasi wanazopewa.Matokeo ya utafiti huu yanabainisha kuwa lugha inaweza kutumiwa na wanawake kama silaha ya kupinga dhuluma ya kijinsia, na kwamba uwezo wa mwanamke kukabiliana na athari za lugha dhalishi unategemea uelewa wake wa matumizi ya lugha kama zana ya kujitetea, kubadili simulizi, na kujenga nguvu ya kijamii.Utafiti huu una mchango muhimu katika taaluma ya lugha na jinsia, hasa kwa kuelekeza mjadala kwa namna ambavyo wanawake wanaweza kujinasua kutoka kwa dhuluma za kimatamshi, na badala yake kutumia lugha kama ngao ya maendeleo na usawa. UTM imethibitisha uwezo wake kama chombo kinachofichua nguvu za kijamii zilizojificha katika matini, na hivyo kusaidia kuelewa mikakati inayotumiwa na wanawake katika kujinasua kutoka kwenye mifumo ya kilinguistiki dhalishi..</p>2025-09-18T14:48:53+00:00##submission.copyrightStatement##https://journals.eanso.org/index.php/eajss/article/view/3781Uchambuzi wa Mtazamo wa Jamii Kuhusu Matumizi ya Taswira ya Mwanamke katika Nyimbo za Singeli za Wasanii Amani Hamisi (Manfongo) na Selemani Jabiri (Msagasumu) kwa Jamii ya Watanzania2025-10-14T07:26:26+00:00Neema Alson Mtwaleneemaalsonmtwale@gmail.comJacob Leopardneemaalsonmtwale@gmail.comHadija Jilalaneemaalsonmtwale@gmail.com<p>Makala hii inahusu Uchambuzi wa mtazamo wa jamii kuhusu matumizi ya taswira ya mwanamke katika nyimbo za singeli za wasanii Amani Hamisi (Manfongo) na Selemani Jabiri (Msagasumu) kwa jamii ya Watanzania. Utafiti ulifanyika katika Maktaba ya Chuo Kikuu Huria, Tawi la Mbeya, ambapo sampuli ya nyimbo saba kutoka kwa wasanii wawili ilichaguliwa kwa usampulishaji lengwa kutokana na umaarufu na maudhui yanayomhusu mwanamke. Utafiti huu umeongozwa na Nadharia ya Ufeministi ambayo imewezesha kuchambua namna wanawake wanavyosawiriwa na changamoto wanazokabiliana nazo katika jamii kinzani za kijinsia. Matokeo ya utafiti yamebainisha kuwa nyimbo teule zinatumia taswira mbalimbali za mwanamke kama vile “msambwanda”, “kitasa”, “chura” na “mkufunzi” ambazo zimegawanyika katika makundi ya taswira za uoni, masikizi, mguso na kimaaelezo. Taswira hizi zina uhalisia wa maisha ya wanawake katika jamii ya Kiswahili. Utafiti pia ulibaini kuwa baadhi ya taswira hizo zinakubalika kijamii kwa kuwa zinadumisha maadili, kuonya na kuelimisha, ilhali nyingine zinapotosha kwa kudhalilisha wanawake na kuendeleza mitazamo hasi. Aidha, dhima za taswira hizo zimehusisha kuonyesha maisha halisi ya mtaani na kijamii, kuonesha umuhimu wa familia, kudhalilisha wanawake wanaojiuza na kuonesha madhara ya kushindwa kujitawala. Utafiti umehitimisha kuwa nyimbo za singeli ni nyenzo muhimu ya fasihi ya Kiswahili, lakini zinahitaji mwelekeo chanya wa kijinsia. Mapendekezo yametolewa kwa wasanii, jamii na taasisi za utamaduni kuhakikisha matumizi ya taswira yanazingatia maadili, utu na usawa wa kijinsia.</p>2025-10-08T15:37:52+00:00##submission.copyrightStatement##https://journals.eanso.org/index.php/eajss/article/view/3783Sababu za Kutokea kwa Ndoa za Mitala katika Riwaya Teule- Barua Ndefu Kama Hii (1980), Takadini (2004) na Paradiso (2014) katika Mpito wa Wakati2025-10-09T04:06:41+00:00Agnes Kwamboka Ometesamwelngetich001@gmail.comJesse Joseph Murithi, PhDJesse.murithi@ku.ac.ke<p>Ndoa za mitala zimekuwepo katika jamii zetu kwa kipindi kirefu sana. Walio katika ndoa hizi huchochewa na sababu tofauti tofauti. Kwa kuwa suala hili limekita mizizi sawasawa katika jamii zetu, waandishi mbalimbali wa kazi za fasihi wameweza kuliangazia katika kazi zao kwa kipindi kirefu. Ni kutokana na hali hii, makala hii inaangazia kwa kina sababu za kutokea kwa ndoa hizi kwa mujibu wa riwaya tatu teule - Riwaya ya Barua Ndefu Kama Hii iliyoandikwa na Mariama Bâ (1980), Takadini ya Ben Hanson (2004) na Paradiso ya John Habwe (2014). Riwaya hizi ziliteuliwa kimakusudi kwa kuwa japo zimeandikwa katika vipindi tofauti, zote zimeangazia vyema suala hili la ndoa za mitala. Hii inabainisha kuwa ndoa hizi zingali na umaarufu katika jamii zetu. Utafiti huu uliongozwa na nadharia ya Uhalisia ya Villanueva (1997). Utafiti ulifanywa maktabani na mtandaoni. Data ya msingi ilipatikana kwa kuvitalii vitabu vilivyoteuliwa kisha kuipanga katika makundi na kuichanganua kwa kuzingatia malengo ya utafiti. Aidha, utafiti ulinufaishwa kwa kuzisoma na kuzihakiki kazi zinazohusiana na suala hili kwenye majarida, makala ya magazeti, tasnifu, vitabu na machapisho mengine. Matokeo yaliwasilishwa kupitia maelezo. Ingawa kuna mabadiliko makubwa katika mpito wa wakati, utafiti huu ulibaini kuwa sababu za kutokea kwa ndoa hizi hazijabadilika sana. Baadhi ya sababu hizi ni; utamaduni katika jamii, shinikizo la kulipiza kisasi, ubabedume, mafundisho ya kidini, ari ya kupata utajiri, viongozi kuwavutia wanawake, utasa au kukosa mtoto wa kiume, mabadiliko ya kimajukumu katika ndoa, wanandoa kutengana kutokana na ajira na hali ya wanandoa kutotosheka kimapenzi. Waandishi, watafiti na wadau wengine wa kazi za fasihi watafaidika na makala hii kwa kuwa yameviangazia kwa kina visababishi vya suala hili la mitala. Aidha, matokeo ya kazi hii yataweza kuwafaa wanaojihusisha na masuala ya kijamii kupata mwanga zaidi kuhusu mabadiliko katika suala la mitala miongoni mwa wanajamii kote ulimwenguni.</p>2025-10-09T03:51:46+00:00##submission.copyrightStatement##https://journals.eanso.org/index.php/eajss/article/view/3854Uhakiki wa Mabadiliko ya Kisemantiki katika Baadhi ya Vitenzi vya Kikamba2025-10-20T18:50:59+00:00Angela Nthenya Musyokaaggymutuku76@gmail.comJohn Musyoka Mutuaaggymutuku76@gmail.comVifu Said Makotiaggymutuku76@gmail.com<p>Mabadiliko ya maana katika lugha ni jambo lisiloweza kuepukika kwa kuwa lugha ni kiungo hai kinachoathiriwa na wakati, mazingira, jamii na muktadha wa matumizi. Kadri muda unavyopita, maana zaidi huingizwa katika lugha na kusababisha maana za maneno hayo kubadilika. Neno linaweza kudumisha maana ya msingi huku pia likiendelea kupata maana nyingine mpya zinazoibuliwa na mazingira mapya ya kisemantiki (Ullman, 1972). Mabadiliko ya maana yanapotokea huathiri mawasiliano iwapo wazungumzaji wa lugha hawatafahamu mabadiliko yaliyoathiri lugha wanayoitumia. Katika lugha ya Kikamba, mabadiliko ya kisemantiki yanaonekana hasa kupitia matini za zamani kama Biblia ya Kikamba ya mwaka 1974 (Mbivilia). Baadhi ya msamiati uliotumiwa katika Biblia hii hautumiwi katika mazungumzo ya kawaida ingawa Biblia yenyewe inasomwa hadi leo makanisani, nyumbani na katika hafla za arusi au mazishi. Waumini wengi wanaosikiliza mahubiri kutoka Biblia hizo hawaelewi maana iliyokusudiwa ya baadhi ya vitenzi. Hali hii huleta utata wa mawasiliano kati ya vizazi. Makala hii imechunguza mabadiliko ya kisemantiki ya vitenzi kumi vilivyochaguliwa kutoka Mbivilia (1974). Nadharia ya Dhana imetumika kutathmini maana ya vitenzi hivyo kwa kutumia usaili wa wazee kumi na watoto kumi. Utafiti umefanywa kwa njia ya mahojiano na usomaji maktabani. Matokeo yameonyesha kuwa baadhi ya vitenzi vimepanuka maana, vingine vimebanwa, baadhi ya maana zimepotoshwa na zingine zimetoweka kabisa. Vitenzi kama vile vuta na mumunya vimepata maana mpya huku maana ya awali ikisahaulika. Watoto wa sasa hawatambui maana asilia ya vitenzi hivyo. Jambo hili linaashiria pengo la kiisimu kati ya vizazi. Matokeo ya utafiti huu yanakusudiwa kuwasaidia wasomaji wa matini za Kikamba hususan zilizoandikwa au kuchapishwa kabla ya karne ya ishirini na moja kuelewa maana ya vitenzi ili kuondoa utata wa mawasiliano baina ya vizazi</p>2025-10-20T00:00:00+00:00##submission.copyrightStatement##https://journals.eanso.org/index.php/eajss/article/view/3857Uhakiki wa Mtindo katika Riwaya ya Kiswahili: Mifano Riwaya za Kidagaa Kimemwozea na Chozi la Heri2025-10-20T18:50:59+00:00Rose Kawira, PhDfaithkathure@yahoo.co.ukFaith Kathure Murugufaithkathure@yahoo.co.uk<p>Utafiti huu ulikusudia kuchanganua matumizi ya mtindo katika riwaya za Kidagaa Kimemwozea (2012) ya Ken Walibora na Chozi la Heri (2017) ya Assumpta Matei. Mtafiti aliongozwa na malengo mahususi matatu ambayo ni; kuchunguza baadhi ya mbinu za kimtindo, kujadili athari za mbinu za kimtindo katika usawiri wa wahusika na kujadili mchango wa mbinu teule katika ujenzi wa maudhui kwa mujibu wa riwaya teule. Mtafiti alitembelea maktaba ili kusoma kazi za waandishi zilizojikta kwenye mada zilizo na uhusiano na mbinu za lugha za fasihi. Mtafiti alisoma tasnifu, magazeti, majarida pamoja na vitabu vya waandishi tofauti. Mtafiti pia alisakura kwenye mitandao ili kuboresha data yake kwa kuangazia kazi za wasomi tofauti kuhusiana na mada kusudiwa. Utafiti huu uliongozwa na Nadharia ya Umitindo iliyoasisiwa na Buffon mnamo mwaka wa 1930. Mihimili minne ya nadharia hii ilitumika kuchunguza matumizi ya mbinu tofauti za mtindo, namna zilivyotumika katika usawiri wa wahusika na kisha mchango wa mbinu angaziwa katika ujenzi wa maudhui. Mbinu ziliochunguzwa ni sadfa, mbinu rejeshi, hadithi ndani ya hadithi, tashbihi na majazi. Data ilichanganuliwa na kuwasilishwa kimaelezo kwa kujikita kwenye mihimili ifaayo. Utafiti huu utarutubisha maarifa kwa wasomaji wanaovutiwa na mbinu tofauti za lugha zilizotumika katika tungo. Pia, utafiti huu utawafaidi walimu na wahadhiri kwa kuwa na uelewa zaidi kuhusu mtindo wa kifasihi wanapofundisha wanafunzi wao. Vivyo hivyo, utafiti huu utafaidi watafiti wa baadaye watakaokuwa na nia ya kuchunguza mitindo katika kazi za fasihi. Hatimaye, utafiti huu utatumika kama marejeleo kwa kazi za baadaye za ubunifu na haswa zile zinazohusiana na mtindo katika fasihi</p>2025-10-20T00:00:00+00:00##submission.copyrightStatement##https://journals.eanso.org/index.php/eajss/article/view/3865Kiswahili katika TEHAMA: Tafsiri kama Daraja la Upatikanaji wa Maarifa2025-10-21T16:58:15+00:00Raphael Mwaura Gacheiyargacheiya@egerton.ac.ke<p>Katika enzi ya kidijitali, tafsiri ya Kiswahili inachukua nafasi muhimu katika kuwezesha upatikanaji wa maarifa kupitia Teknolojia ya Habari na Mawasiliano (TEHAMA). Makala hii inajadili jinsi tafsiri ya Kiswahili inavyotumika kama daraja kati ya watumiaji na maarifa ya kidijitali, kwa kutumia Nadharia ya Ufikiaji wa Maarifa na Nadharia ya Mawasiliano katika Tafsiri. Kwa kutumia mbinu ya uchambuzi wa maudhui na mahojiano ya kina na wataalamu wa lugha, TEHAMA, na watumiaji wa majukwaa ya kidijitali, ilibainika kuwa tafsiri ya Kiswahili hairahisishi tu mawasiliano, bali pia huchochea usawa wa maarifa, ukuzaji wa lugha katika nyanja za kiteknolojia, na ujumuishaji wa jamii katika maendeleo ya kidijitali. Hata hivyo, changamoto kama ukosefu wa istilahi sanifu na ushirikiano mdogo kati ya wataalamu wa lugha na teknolojia huathiri ubora wa tafsiri. Makala inapendekeza uwekezaji katika tafsiri bora, maendeleo ya istilahi bunifu, na ushirikiano wa kitaaluma ili kuhakikisha Kiswahili kinapata nafasi endelevu na thabiti katika mazingira ya TEHAMA</p>2025-10-21T16:54:35+00:00##submission.copyrightStatement##https://journals.eanso.org/index.php/eajss/article/view/3870Michakato ya Kisemantiki Iliyoathiri Nomino za Kikamba Zilizoteuliwa katika Biblia2025-10-24T13:25:03+00:00Angela Nthenya Musyokaggymutuku76@gmail.comVifu Said Makotiaggymutuku76@gmail.comJohn Musyoka Mutuaaggymutuku76@gmail.com<p>Kipengele cha maana ni muhimu sana katika msamiati wa lugha kwa kuwa hufanikisha mawasiliano. Maana ya neno inapobadilika kwa namna yoyote ile huathiri mchakato mzima wa mawasiliano (Crowley, 1997). Iwapo maneno yanayotumiwa na mzungumzaji hayaeleweki na mpokeaji wa ujumbe, basi wawili hao hawataelewana. Biblia za Kikamba zilizoandikwa au kuchapishwa katika karne zilizopita zina maneno ambayo hayaeleweki na kizazi cha karne hii ya ishirini na moja. Biblia hizo zinazidi kutumiwa katika mahubiri makanisani na katika hafla mbalimbali kama vile harusi na mazishi. Makala hii imechunguza michakato ya kisemantiki inayohusishwa na mabadiliko ya maana kwa kuangalia jinsi nomino teule zilivyobadilika maana. Michakato hii imepatikana baada ya kuwahoji wazee na watoto kuhusu maana ya maneno teule ya Kikamba yaliyodondolewa kwenye Biblia ya Kikamba iliyochapishwa mwaka 1974. Majibu yao yamebainisha kwamba maana za nomino hizo zimepitia michakato ya mabadiliko ya maana kama vile upanuzi, ubanaji, usogezi, kusambaratika, tasfida, utowekaji na kuhamisha maana. Nadharia mbili zimetumika katika utafiti huu; Nadharia ya Dhana na nadharia ya Nyanja za Kisemantiki. Nadharia ya dhana imemwezesha mtafiti kupata maana asilia na maana za sasa za nomino kama dhana iliyoibuka akilini mwa wahojiwa baada ya nomino hizo kutamkwa au kuandikwa. Nadharia ya Nyanja za Kisemantiki imetumiwa kubainisha nomino ambazo zilihusiana kimaana na zingine kwa kuwa zilikuwa katika nyanja sawa za maana (Lyons, 1999). Matokeo ya utafiti huu yanakusudiwa kuwawezesha wasomaji wa Biblia za Kikamba kuelewa maana katika Biblia zilizotangulia hasa zile za miaka ya sabini (1970s) na kupunguza utata wa kimawasiliano baina ya wahubiri na waumini wa kizazi cha karne hii ya ishirini na moja. Aidha, wataalamu wa lugha wataweza kuandika kamusi ya visawe na kamusi ya maana za maneno kama inavyoeleweka katika jamii ya leo.</p>2025-10-24T13:23:37+00:00##submission.copyrightStatement##