TY - JOUR AU - Paul I. Bundi AU - Onesmus Ntiba AU - Allan Mugambi PY - 2022/10/12 Y2 - 2024/03/28 TI - Mabadiliko Ya Hadithi Fupi Teule Za Kiswahili : Mkabala Wa Usasaleo JF - Jarida la Afrika Mashariki la Masomo ya Kiswahili JA - JAMMK VL - 5 IS - 2 SE - Makala DO - 10.37284/jammk.5.2.882 UR - https://journals.eanso.org/index.php/eajss/article/view/882 AB - Makala hii inachunguza mabadiliko katika hadithi fupi kwa mkabala wa usasaleo. Inaangazia athari za usasaleo katika hadithi fupi za kimapokeo. Kwa kuwa athari ya kiusasaleo inaendelea kujitokeza katika hadithi fupi za kisasa kila kukicha, kulikuwepo na haja ya kutafiti juu ya mabadiliko haya. Katika makala hii mtafiti alichunguza vile baadhi ya hadithi zilivyoegemea uhalisia na umapokeo na jinsi waandishi wengine walivyotumia majaribio ya kimuundo, kimtindo na kimaudhui kuandika hadithi fupi za kisasa. Mtafiti alikusanya data katika diwani tatu za hadithi fupi za: Mayai Waziri wa Maradhi na Hadithi Nyingine, Mizungu ya Manabii na Hadithi Nyingine na Homa ya Nyumbani na Hadithi Nyingine. Data iliteuliwa, kupangwa na kujadiliwa kulingana na maswali na madhumuni ya utafiti. Makala hii iliongozwa na nadharia ya umuundoleo iliyoasisiwa na Jacques Derrida na Michel Foucalt mwaka wa 1960. Madhumuni ya utafiti huu yalikuwa: Kubainisha mabadiliko ya kimuundo ya kiusasaleo katika hadithi fupi teule za Kiswahili, kudhihirisha mabadiliko ya kimtindo yaliyosababishwa na usasaleo katika hadithi fupi teule za Kiswahili na kufafanua mabadiliko ya kimaudhui yaliyotokana na usasaleo katika hadithi fupi teule za Kiswahili. Katika hadithi sita teule zenye mbinu za kiusasaleo waandishi walitumia mabadiliko majaribio na upya katika muundo mtindo na maudhui. Sampuli maksudi ilitumika kuteua hadithi zilizofaa utafiti huu. Madhumuni na maswali ya utafiti yalitumika kuteua kupanga na kueleza data. Matokeo ya utafiti yalitolewa kimaelezo katika sura ya nne, tano na sita na hitimisha kutolewa katika sura ya saba. Matokeo ya utafiti yanatarajiwa kufaa wanafunzi wa fasihi wa shule za upili,watafiti wa baadaye, wahakiki na wasomi wa fasihi kwa kuwapa uelewa mpana wa mabadiliko yanayotokea katika uandikaji wa hadithi fupi za Kisasa. Zaidi ya haya, utafiti huu ulichangia kuziba pengo lililopo katika utafiti juu ya mabadiliko katika hadithi fupi mkabala wa usasaleo. Maarifa yanayotokana na utafiti huu ni mchango muhimu katika fasihi andishi hasa hadithi fupi za Kiswahili. ER -