TY - JOUR AU - Joseph Ismail PY - 2020/06/09 Y2 - 2024/03/29 TI - Mchango wa Tasinia ya Sheria katika Ukuzaji na Uenezaji wa Kiswahili Tanzania: Mifano kutoka Mahakama ya Tanzania na Taasisi za Wadau wa Sheria JF - Jarida la Afrika Mashariki la Masomo ya Kiswahili JA - JAMMK VL - 2 IS - 2 SE - Makala DO - 10.37284/eajss.2.2.160 UR - https://journals.eanso.org/index.php/eajss/article/view/160 AB - Kukua na kuenea kwa lugha ya Kiswahili nchini Tanzania kunategemea mambo mbalimbali kama vile kutumika katika maeneo na mifumo rasmi kwenye jamii husika. Historia ya lugha ya Kiswahili inaonekana kukua tangu wakati wa biashara ya watumwa, Waarabu, kipindi cha ukoloni wa Wajerumani na kipindi cha ukoloni wa Waingereza. Harakati za kusanifisha lugha ya Kiswahili kwa hatua mbalimbali za usanifishaji wake (1928- 1930) zilichapuza kukua na kusambaa kwa lugha ya Kiswahili. Baada ya uhuru wa Tanzania, Tanganyika wakati huo, lugha ya Kiswahili ilizidi kukua hasa baada ya serikali katika mwaka 1962 kuifanya kuwa lugha ya Taifa na lugha rasmi ya mawasiliano katika shughuli mbalimbali za kiserikali na zisizo za kiserikali. Vyombo mbalimbali vya kukuza Kiswahili viliundwa kama vile Baraza la Kiswahili la Tanzania (BAKITA), Taasisi ya Ukuzaji wa Kiswahili (TUKI) kutokana na kamati iliyokuwa ya usanifishaji wa lugha ya Kiswahili ya Afrika Mashariki na Idara ya Kiswahili ya Chuo Kikuu cha Dar es salaam, kuvitaja kwa uchache. Idara ya Kiswahili ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam ilikuwa na jukumu la kufundisha somo la Kiswahili na wataalamu wake kuandika masuala mbalimbali ya lugha ya Kiswahili. Mazoea yamekuwa kuviangalia vyombo hivi na serikali kwa ujumla kama ndio vyombo pekee vyenye wajibu wa kukuza na kuendeleza lugha ya Kiswahili Tanzania. Tukiachilia mbali vyombo hivi tulivyovitaja, yapo maeneo mengine yanayoweza kukuza na kuendeleza lugha ya Kiswahili ambayo ama hayajaangaliwa kwa kiasi cha kutosha au yamesahaulika. Moja ya maeneo ambayo matumizi ya lugha ya Kiswahili yanaweza kusukuma kukua na kuenea kwake ni eneo la tasinia ya sheria. Lengo la makala haya ni kubainisha namna tasinia ya sheria na taasisi za sheria zinavyosaidia kukua na kuenea kwa Kiswahili nchini Tanzania.  ER -