Tathmini ya Historia ya Mwafrika kupitia Tamthilia Teule za Emmanuel Mbogo; Shujaa Mirambo (2021) na Malkia Bibi Titi Mohammed (2018)

  • Cecilia Kaari Ntabathia Chuo Kikuu cha Kenyatta
  • Richard Makhanu Wafula Chuo Kikuu cha Kenyatta
Keywords: Mwafrika, Tathmini, Usawiri, Tabaini, Kusanisi
Sambaza Makala:

Ikisiri

Makala hii imeshughulikia tathmini ya historia ya Mwafrika kupitia tamthilia teule za Emmanuel Mbogo; Shujaa Mirambo (2021) na Malkia Bibi Titi Mohammed (2018). Suala la historia na fasihi limeshughulikiwa na watafiti mbalimbali ingawa kwa mitazamo iliyo tofautitofauti. Nasimiyu (2013), alitathmini namna mazingira ya kihistoria na ya kijamii yameathiri uwasilishaji wa maudhui katika Diwani ya Dhifa. Munyao (2017) naye alichunguza jinsi taaluma za historia na fasihi huingiliana kwa kuuhakiki Utenzi wa Nchuu Cwavo yapo Tini mwa Irara. Ndung’u 2023 alichunguza athari za kihistoria katika ukuaji wa riwaya za Nyongo Mkalia Ini na Mafamba. Usomi na udurusu wa kina kuhusu yaliyoandikwa kuhusu mada umebainisha kuwa, hakuna mtafiti aliyewahi kuitathmini historia ya Mwafrika hasa kwa kuzitumikiza tamthilia za Emmanuel Mbogo; Shujaa Mirambo na Malkia Bibi Titi Mohammed. Watafiti mbalimballi walijishughulisha na masuala ya mikinzano na mivutano ya vizazi, masuala ya kijinsia, kuupiga vita ufisadi na kuyatalii masuala ya tanzia, bali hawakujihusisha na urekebishaji wa historia ya Mwafrika. Kama walifanya hivyo, ni kwa uchache. Pana haja ya kusisitiza kuhusu kusahihisha mitazamo hasi iliyotokana na ukoloni na Mwafrika mwenyewe wa kisasa juu ya Mwafrika kama mkazi wa bara la Afrika. Makala hii imeongozwa na nadharia za Upembuzi na Uhalisia. Nadharia ya Upembuzi iliasisiwa katika karne ya 19 na Mjerumani kwa jina Hegel. Alidai kwamba, lengo muhimu la upembuzi ni kuyachambua masuala yalivyo na kuyadhihirisha kwa nia ya kuondoa mivutano na mikwaruzano kati ya masuala mbalimbali. Uhalisia ni uwasilishaji wa vitu, vitendo na hali za kijamii kama zilivyo bila kuhusisha udhahania. Hutumiwa kuainisha tapo la fasihi ya karne ya 19 na huwa ni uzingativu wa vitu halisi vinavyobainika kupitia mishipa ya utambuzi wa binadamu. Data iliyotumiwa ilitolewa katika maktaba ambako tamthilia teule, makala, magazeti, majarida na vitabu vinavyohusiana na mada husika vilisomwa na kuchambuliwa kwa undani. Matokeo yamewasilishwa na dondoo mwafaka kutoka tamthilia zilizoteuliwa zikaonyeshwa. Matokeo ya utafiti huu yamebainisha kwamba, tamthilia za Shujaa Mirambo na Malkia Bibi Titi Mohammed zimejaribu kuiboresha picha ya kiongozi wa Kiafrika na mwanamke wa Kiafrika. Ili kuyafanikisha malengo yake, mwandishi alitumia mbinu kama vile majigambo, majibizano, nyimbo na hata jazanda. Katika tamthilia ya Malkia Bibi Titi Mohammed, picha ya Mwafrika inaboreshwa kwa mbinu za kisanaa kama nyimbo na ushairi, motifu ya safari, mjadala, jazanda, wajumbe na barua.

Upakuaji

Bado hatuna takwimu za upakuaji.

Marejeleo

BAKIZA (2010). Kamusi ya Kiswahili Fasaha. Nairobi;. Oxford University Press.

Basden, G.T. (1921). Among The Ibos of Nigeria. Routledge.

Berger, M. (1977). Real and Imagined Worlds. Cambridge, Massachusetts: Harvard University Press.

Churchill, W. (2015). My African Journey. Bloomsbury Publishing.

Conrad, J. (1899). Heart of Darkness. United Kingdom: Blackwood’s Magazine.

Craig, D. (1975). Marxists on Literature. An Anthology. Handsworth: Penguin.

Fanon, F. (1961). The Wretched of the Earth. Vol.36. New York: Grove Press.

Fanon, F. (1952). Black Skins White Masks. London: Paladin.

Hegel, G. W. F. (1956). The Philosophy of History. New York: Dover Publications.

Hegel, G.W.F. (1837). The Philosophy of History. Dover Publications.

Lukacs, G. (1974). The Theory of the Novel: “A Historico-Philosophical Essay on the Forms of Great Epic Literature.” London: The MIT Press.

Mbogo, E. (2021). Shujaa Mirambo. Africa Proper Education Network.

Mbogo, E. (2018). Malkia Bibi Titi Mohammed. Africa Proper Education Network.

Njogu, K na Chimerah, R. (1999). Ufundishaji wa Fasihi: Nadharia na Mbinu. Nairobi: Jomo Kenyatta Foundation.

Munyao, R. M. (2017). Mwingiliano wa Fasihi na Historia katika Utenzi wa Nchuu Cwavo Yapo Tini mwa Irara; Tasnifu ya Uzamili. Chuo Kikuu cha Nairobi.

Nasimiyu, C. (2008). Athari za Mazingira ya Kihistoria na Kijamii Katika Uwasilishaji wa Maudhui katika Diwani ya Dhifa. Tasnifu ya Uzamili, Chuo Kikuu cha Kenyatta.

Ndung’u, B. W. (2003). Athari za Matukio ya Kihistoria katika Riwaya za Nyongo Mkalia Ini na Mafamba. Tasnifu ya Uzamili, Chuo Kikuu cha Kenyatta. (Haijachapishwa).

Njogu, K. na Chimerah, R. (1999). Ufundishaji wa Fasihi, Nadharia na Mbinu. Nairobi: Jomo Kenyatta Foundation.

Nochlin, L. (2018). Misere, The Visual Representation of Misery in 19th Century. New York: Thames and Hudson.

Ohly, R. (2005). Historical Approach to Swahili Literature: As Here to Fore an Open Question. Kiswahili Juzuu la 68 Dar es Salaam; TUKI 2005.

Roper, T. (1992). “The Trevor-Roper Trap” or “The Imperialism of History”: An Essay. United Kingdom: Cambridge University Press.

Said, E. (1977). Orientalism. The Georgia Review, 31(1), 162-206.

Soo, F. (1981). Mao Tse-Tung’s Theory of Dialectic. London: D. Reidel Publishing Company.

Wafula, R. M. na Njogu, K. (2007). Nadharia za Uhakiki wa Fasihi. Nairobi: Jomo Kenyatta Foundation.

Wafula, R.M. (1999). Uhakiki wa Tamthilia: Historia na Maendelo yake. Nairobi: Jomo Kenyatta Foundation.

Wamitila, K. W. (2003). Kamusi ya Fasihi Istilahi na Nadharia. Nairobi. Focus Books Publishers.

Yonah, Y. (1999). “Ubi Patria-Ibi Bene.” The Scope and Limits of Rousseaue’s Patriotic Education. Studies in Education Philosophy, 18(6), 365-388.

Tarehe ya Uchapishaji
1 December, 2025
Jinsi ya Kunukuu
Ntabathia, C., & Wafula, R. (2025). Tathmini ya Historia ya Mwafrika kupitia Tamthilia Teule za Emmanuel Mbogo; Shujaa Mirambo (2021) na Malkia Bibi Titi Mohammed (2018). Jarida La Afrika Mashariki La Masomo Ya Kiswahili, 8(3), 144-155. https://doi.org/10.37284/jammk.8.3.4097

Makala zilizo somwa zaidi kama hii.