Uchambuzi wa Stailikia za Ufupishaji katika Mtandao wa WhatsApp

  • Winifrida Moshi Chuo kikuu Huria cha Tanzania
Keywords: Uchambuzi, Ufupishaji, WhatsApp, Muundo, Dodoso, Mwanza, Mitandao
Sambaza Makala:

Ikisiri

Utafiti huu umeshughulikia “Uchambuzi wa Stailikia za Ufupishaji katika mtandao wa WhatsApp na mchango wake katika ukuaji wa lugha ya Kiswahili. Utafiti huu umetumia muundo mseto, wa kitakwimu na wa kimaelezo. Sampuli iliteuliwa kwa kutumia mbinu ya usampulishaji nasibu sahili ili kuweza kupata data za utafiti. Utafiti huu ulifanyika mkoani Mwanza katika Chuo Kikuu cha Mtakatifu Agustino kilichopo Wilaya ya Nyamagana katika jiji la Mwanza. Nadharia iliyotumika katika utafiti huu ni Nadharia ya “Uchanganuzi Tahakiki Usemi”. Utafiti huu ulikusanya data kutoka uwandani, mbinu iliyotumika kukusanya data ni mbinu ya dodoso.  Matokeo ya utafiti yalionyesha kuwa, staili ya ufupishaji katika mtandao wa WhatsApp inayotumiwa na watu wengi ni ya kudondosha baadhi ya herufi katika neno, kwani ni 77% ya watafitiwa wote waliojibu swali hili hudondosha herufi wanapofupisha maneno. Pia, matokeo yalionyesha kuwa mtandao wa WhatsApp ni jukwaa ambalo limesaidia kukua na kuenea kwa Kiswahili miongoni mwa watumiaji kwa kuwa mtandao huu hutumiwa na watu mbalimbali.  Mapendekezo yanatolewa kwa Taasisi inayochunguza na kukuza Kiswahili kuvisanifisha vifupisho vya maneno vinavyotumika katika mitandao ya kijamii kwani  ni vigumu sana kudhibiti matumizi ya vifupisho kwa kuwa mawasiliano ni uhuru wa mtumiaji na anawasiliana kwa staili anayopenda yeye. Kwa watumiaji wa lugha ya kiswahili, wanapaswa kutofautisha matumizi ya lugha rasma na lugha ya kawaida ili kuepuka kuchanganya matumizi hayo  kwa kuwa watumiaji wengi wanapofupisha au kuandika maneno kimtandao hawafuati sifa za konsonanti na vokali wao huandika konsonanti mbili zikifuatana au konsonanti peke au vokali pekee. Wanaunda na kuandika maneno kulingana na jinsi yanavyokaribiana au kuhusiana kisauti. Wakati mwingine wanaacha silabi fulani katika neno kwa sababu wao wanaamini kuwa maana ya neno huweza kuwakilishwa bila kuwepo kwa fonimu fulani.

Upakuaji

Bado hatuna takwimu za upakuaji.

Marejeleo

Al-Khatibu, M. & Sabbah, E. (2008). Language choice in mobile text message among Jordanian University students. Sky Journal of Linguistics, 3, 37-65.

Batul, F. (2009). Chatspeak: Linguistic evolution or devolution. Pergamon Press.

Brody, L.T. and Geigle, P.R. (2009). Aquatic Exercise for Rehabilitation and Training. Champaign.

Crystal, D. (2008). Texting: The gr8 db8. Oxford University Press.

Fagan, J.E. & Desai, C.M. (2003). Site search and instant messaging reference: A comparative study. Intemet Reference Services Quarterly, 8(1/2), 167-182

Goumi, A. (2011). SMS Length and Function: A comparative study of 13 to 18 year – old girls and boys. European Review of Applied Psychology, 61(4), 175 – 184.

Ingo, P. (2003). Word formation in English. Cambridge University Press.

Kothari, C. R. (2009). Research Methodology: Methods and Techniques. New Age Internation Publishers.

Matinde, R. (2012). Dafina ya lugha. Serengeti Educational Publishers Ltd. McGregror, L. T. na Mitstifer, D.I (2003). Critical Science and Critical Discourse. Nu FORUM Analysis. 15(1). Kappa Omicron.

Ong'onda, N. A., Matu, P. M., Oloo, P. A. (2011). Prosodic features in Facebook Communication. Sciedu Press.

Rubanza, Y. I. (1996). Mofolojia ya Kiswahili. Chuo Kikuu Huria cha Tanzania.

Varnhagen, C. K., McFall, G. P., Pugh, N., Routledge, L., Sumida-MacDonald, H., & Kwong, T. E. (2010). Lol: New language and spelling in instant messaging. Reading and writing, 23, 719-733.

Werry, C. (1996). Linguistic and interactional features of Internet relay chat. In S. C.Herring (Ed.), Computer-mediated communication: Linguistic, social, and cross cultural perspectives. Amsterdam: John Benjamins.

Williman, N. (2011). Research Methods: The Basic. Routledge Taylor & Francis Group.

Tarehe ya Uchapishaji
25 November, 2025
Jinsi ya Kunukuu
Moshi, W. (2025). Uchambuzi wa Stailikia za Ufupishaji katika Mtandao wa WhatsApp. Jarida La Afrika Mashariki La Masomo Ya Kiswahili, 8(3), 117-125. https://doi.org/10.37284/jammk.8.3.4069