Sababu za Kuwepo kwa Mapengo katika Violezofaridi katika Lugha ya Kiswahili

  • Naomi Ndumba Kimonye, PhD Chuo Kikuu cha Kenyatta
  • Peter Githinji Chuo Kikuu cha Kenyatta
  • Leonard Chacha Mwita Chuo Kikuu cha Kenyatta
Keywords: Kiolezofaridi, Kiangami, Mashartizuizi, Mshindani, Pengo, Umbotokeo
Sambaza Makala:

Ikisiri

Vipashio vya lugha vinapokosa kuzingatia ruwaza iliyopo, huwa kuna sababu muhimu ya kufanya hivyo. Makala haya yanalenga kubainisha sababu za kuwepo kwa mapengo katika violezofaridi katika lugha ya Kiswahili. Kiolezofaridi (paradigm) ni mfumo wa miundo ya kisarufi. Kuna wakati ambapo vipashio vya lugha vinakubalika licha ya kuwa vimekiuka kanuni za lugha pia, vipashio vingine vinakosa kukubalika licha ya kuzingatia sheria. Hali hii ndio tunaita pengo la kiolezofaridi. Katika makala hii, tumeweka wazi baadhi ya mapengo ya kiolezofaridi katika lugha ya Kiswahili na kisha kueleza sababu ya kuwepo kwa mapengo hayo. Nadharia ya Kiolezofaridi Bora (Optimal Paradigms) iliyoasisiwa na McCarthy (2005) ndiyo iliyotumika. Nadharia hii hujikita katika mtagusano wa mashartizuizi ya uadilifu na uziada katika kuteua mshindi. Kwa upande wake, mashartizuizi ndiyo nguzo ya kiolezofaridi ambacho huteua mshindi kutoka kwa maumboshindani anuawai ambayo yanaweza kuzalishwa na kanuni za kisarufi za lugha husika. Data ya utafiti ilipatikana maktabani na mtandaoni. Watafiti walichambua vitabu vya lugha ya Kiswahili ambavyo vimechapishwa, tasnifu na pia, makala yaliyochapishwa mtandaoni. Asili ya data ni matini teule za isimu na data yenyewe ni violezofaridi vyenye mapengo. Usampulishaji     dhamirifu ulitumika kuteua kazi za isimu. Data iliteuliwa kimakusudi na kuwasilishwa kwa njia ya maelezo na majedwali. Utafiti huu ulionyesha wazi uwepo wa mapengo kwenye violezofaridi katika lugha ya Kiswahili. Lugha ya Kiswahili huongozwa na sheria kila mara hivyo basi pengo linapotokea huwa kuna sababu

Upakuaji

Bado hatuna takwimu za upakuaji.

Marejeleo

Allan, K. & Burridge, K. (1991). Euphemism and Dysphemism. New York: Oxford University Press.

Albright, A. (2003). A Quantitative Study of Spanish Paradigm Gaps. In West Coast Conference on Formal Linguistics 22 Proceedings, (eds) uk. 1-14. Gina Garding and Mimu Tsujimura. Somerville, MA: Cascadilla Press.

Auwera, J., Olmen, D. & Mon, D. (2019). Cognitive Linguistics: Grammaticalization. Chapter 11. De Gruyter Mouton. https://doi.org/10.1515/9783110626438-011

Crowley, T. & Bowern, C. (2010). An Introduction to Historical Linguistics. London: Oxford

Durken, P. (2014). Borrowed Words: A History of Loanwords in English. Oxford: Oxford University Press.

Gromova, N. (2001). Mara Tena Juu ya Usarufishaji (Suala la Mwana). Swahili Forum VIII 59-65

Harry, H. (1954). Language in Culture. Chicago: The University of Chicago Press.

Hogg, R. and Denison, D. (2006). A History of English Language. Cambridge: Cambridge University Press.

Kager, R. (2004). Optimality Theory. Cambridge: Cambridge University Press.

Katamba, (1985). Mordern Linguistics: Morphology. New York: Palgrave Macmillan.

Lehman, W. (1973). Descriptive Linguistics. New York: Random House.

Massamba, D. (2010). Phonological Theory: History and Development. Dar es Salaam: TUKI.

Massamba, D. P. B. (2011). Maendeleo katika Nadharia ya Fonolojia. Dar es Salaam: Taasisi ya Taaluma za Kiswahili.

McCarthy, J. & Prince, A. (1993). Prosodic Morphology: Constraint Interaction and Satisfaction. Amherst, M.A: University of Massachusetts.

McCarthy, J. (2005). Optimal Paradigms. Boston: University of Massachusetts.

Mgullu, R. (2001). Mtalaa wa Isimu: Fonetiki, Fonolojia na Mofolojia ya Kiswahili Nairobi: Longhorn.

Mwaro, G. (2000). ‘Usayansi wa Istilahi za Isimu ya Kiswahili’. Tasnifu. Chuo Kikuu cha Egerton.

Mwita, L. C. & Malangwa, P. S. (2019). Semantiki. Nairobi: Longhorn Publishers

Nguti, M. (2013). Ulinganishaji wa Matumizi ya Tasfida za Muktadha wa Nyumbani katika Lugha ya Kikamba na Kiswahili. Tasnifu. Chuo Kikuu cha Nairobi.

Ortony, A. (1993). Metaphor and Thought. Camridge: Cambridge University Press.

Pertsova, K. (2005). How Lexical Conservatism Can Lead to Paradigm Gaps. UCLA Working Papers in Linguistics, no11. Califonia.

Prince, A. & Smolensky, P. (1993). Optimality Theory: Constraint Interaction in Generative Grammar. RuCCs-TR-2. ROA-537. 262 COLORADO: University of Colorado at Boulder. rtony, A. (1993). Metaphor and Thought. Camridge: Cambridge University Press.

Rice, C. (2005). Nothing is a Phonological Fact: Gaps and Repairs at the Phonology-morphology Interface. Castl: University of Tromso

Saussure, F. (1959). Course in General Linguistics. New York: Facsimile Publisher.

Tarehe ya Uchapishaji
13 November, 2025
Jinsi ya Kunukuu
Kimonye, N., Githinji, P., & Mwita, L. (2025). Sababu za Kuwepo kwa Mapengo katika Violezofaridi katika Lugha ya Kiswahili. Jarida La Afrika Mashariki La Masomo Ya Kiswahili, 8(3), 66-81. https://doi.org/10.37284/jammk.8.3.3975

Makala zilizo somwa zaidi kama hii.

1 2 > >>