Ujenzi wa Uadiliswhaji wa Watoto katika Jamii: Mifano: Riwaya ya Mshale wa Matumaini na Cheupe na Cheusi

  • Rose Kawira, PhD Chuo Kikuu cha Mount Kenya
  • Jackson Ndung’u, PhD Chuo Kikuu cha KCA
  • Oduor Everlyn Akello Chuo Kikuu cha Mount Kenya
Keywords: Ujenzi wa Uadiliswhaji, Watoto katika Jamii
Sambaza Makala:

Ikisiri

Fasihi huchukua nafasi kubwa katika jamii kwani ni chombo muhimu sana cha kusawiri masuala nyeti yanayofungamana na jamii kwa jumla. Mojawapo ya masuala yanayofungamana na jamii ni lile la maadili. Utafiti huu ulishughulikia nafasi ya fasihi ya watoto katika kuadiliza watoto kama inavyodokezwa katika riwaya teule za Mshale wa Matumaini na Cheupe na Cheusi. Katika utafiti wetu tuliongozwa na nadharia ya maadili iliyoasisiwa na Plato kutoka Ugiriki mnamo mwaka wa 387 kabla ya Kristo na ambayo inalenga kutatua matatizo yanayokumba jamii kwa minajili ya kujenga jamii bora iliyo na maelewano. Lengo kuu la utafiti huu lilikuwa ni kuchunguza vipengele vya maadili katika wahusika watoto kwenye riwaya teule. Data hitajika ilipatikana kwa kusoma riwaya mbili zilizoteuliwa na mtafiti. Vile vile, data ilipatikana katika maktaba za Chuo Kikuu cha Mount Kenya pamoja na Chuo Kikuu cha Jaramogi Oginga Odinga pale ambapo mtafiti alisoma nakala za tasnifu zinazohusiana na mada ya uadilifu, vitabu, magazeti na majarida yaliyo na mada zilizo na uhusiano na mada tafitiwa. Pia, mtafiti alitalii mtandao kwa kusudi la kusaka habari zaidi zinazohusiana na mada za uadilifu katika jamii ya mwanadamu. Utafiti huu ulitumia usampulishaji wa kimaksudi ambapo sampuli lengwa ilikuwa makala zinazohusiana na uadilifu pamoja na riwaya mbili teule. Mbinu ya kimaelezo ilitumika katika kuwasilisha matokeo ya utafiti. Utafiti utafaidi jamii kwa kuiongezea maadili muhimu ya kuikuza. Pia, utakuwa marejeleo kwa taaluma ya fasihi kwa watafiti wa baadaye. Walimu wanaotangamana na wanafunzi watafaidika na upanuzi wa maudhui ya uadilifu na mengine yanayojengwa na vipengele vya maadili haswa wanapotangamana na watoto. Katika mchakato mzima wa utafiti, maadili yote hitajika yalizingatiwa ili kuhakikisha kuwa utafiti ni wazi na wa kuaminika na nyanja zote husika..

Upakuaji

Bado hatuna takwimu za upakuaji.

Marejeleo

Bamwenda, E. (2019). “The Symptoms of the Shift Towards Authoritarian State in Tanzania”. Hhh://doi.org/10.12797//politeja.15.2018.56.08

Gwako, J. (2016). Uchanganuzi Linganishi wa Suala la Maadili kwa Vijana wa Kiume

katika tenzi Mbili: Siraji na Adili. Tasnifu ya Uzamili, Chuo Kikuu cha Nairobi: (Haijachapishwa)

Habwe, J. (2022). Mshale wa Matumaini. Nairobi: Access Publishers Limited.

Mathooko, P. (2007). Isimujamii: Misingi na Nadharia. Nairobi: Njigua Books

Mgogo, Y. (2017). Kuchunguza Hadithi za Wanyika katika Elimu ya Jadi. Tasnifu ya Shahada ya Uzamifu, Chuo Kikuu Huria cha Tanzania.

Muguro, H. (2018). The Theme of Intergrity in Christian Lliterature: An Analysis of Childrens Books. Masters Thesis, Chuo Kikuu cha Kenyatta (Haijachapishwa)

Mwangosi, G. (2019) Kuchunguza Dhamira na Fani katika Nyimbo za Magosi za Jamii ya Tanzania. Tasnifu ya Shahada ya Uzamifu, Chuo Kikuu cha Huria Tanzania.

Naliaka, R. (2012). Hali ya Vijana katika Riwaya ya Vipanya vya Maabara.” Tasnifu ya Uzamili, Chuo Kikuu cha Nairobi: (Haijachapishwa)

Ndalu, A. & Mirikau, A. (2014). Kamusi Teule ya Kiswahili: Kitele cha Lugha. Nairobi: East African Education Publishers.

Nyamemba, R. (2012). Uchanganuzi Linganishi wa jinsi Waandishi katika Tunu ya Ushairi Wanavyoshughulikia Masuala ya Vijana. Tasnifu ya Uzamili, Chuo Kikuu cha Nairobi (Haijachapishwa)

Omar, S. (2016). Fasihi na Jinsia: Mfano Kutoka Nyimbo za Watoto Tanzania Kiswahili Juzu.71, uk. 97-104

Tamir, K. (2021). Maudhui ya Kiisilamu katika Nyimbo Taarab. Tasnifu ya Shahada Uzamifu. Chuo Kikuu Huria cha Tanzania (Haijachapishwa)

Thody, P. (1997). Don’t do it. A Dictionary of the Forbidden. New York: St. Martins Press.

www.sematanzania.org

Wamitila, K.W. (2003). Kamusi ya Fasihi: Istilahi na Nadharia. Nairobi: Focus Publication Ltd.

Watuha, A. (2011). Maudhui ya Waadhi Katika Utenzi wa Adili. Tasnifu ya Uzamili, Chuo Kikuu cha Nairobi (haijachapishwa)

Tarehe ya Uchapishaji
12 November, 2025
Jinsi ya Kunukuu
Kawira, R., Ndung’u, J., & Akello, O. (2025). Ujenzi wa Uadiliswhaji wa Watoto katika Jamii: Mifano: Riwaya ya Mshale wa Matumaini na Cheupe na Cheusi. Jarida La Afrika Mashariki La Masomo Ya Kiswahili, 8(3), 50-65. https://doi.org/10.37284/jammk.8.3.3959