Athari za Maendeleo ya Sayansi na Teknolojia Kwenye Ngano za Jamii ya Wasukuma

  • Janeth M. Balele Chuo Kikuu Huria cha Tanzania
  • Mohamed Omary Maguo Chuo Kikuu Huria cha Tanzania
Keywords: Athari chanye, Sayansi na teknolojia, Athari hasi, Ngano za Kisukuma, Tanzania
Sambaza Makala:

Ikisiri

Makala haya yamelenga kuchunguza athari za maendeleo ya sayansi na teknolojia katika matumizi, uhifadhi, na uendelezaji wa ngano za Kisukuma katika Wilaya ya Kahama, Mkoa wa Shinyanga. Utafiti ulifanyika katika kata nne za Isagehe, Iyenze, Kahama Mjini na Nyandekwa, ukihusisha wazee 38 wenye umri wa zaidi ya miaka 70 walioteuliwa kwa usampulishaji lengwa. Data zilikusanywa kupitia dodoso na mahojiano ya kina, na kuchambuliwa kwa kutumia programu ya SPSS (toleo la 23) na uchambuzi wa maudhui kwa kutumia ATLAS.ti. Matokeo yalionyesha kuwa maendeleo ya sayansi na teknolojia yamechangia katika kuhifadhi na kusambaza ngano za Kisukuma kupitia redio, televisheni, mitandao ya kijamii na maandiko ya kielektroniki. Teknolojia pia imeongeza ubunifu katika usimulizi kupitia filamu, michezo ya kuigiza na majukwaa ya kidijitali, hivyo kukuza utambulisho wa Kisukuma. Hata hivyo, changamoto kama kupungua kwa nafasi ya wazee kama wahifadhi wa maarifa, kudhoofika kwa lugha ya Kisukuma, na kupotea kwa mila ya usimuliaji wa mdomo zilibainika. Aidha, maudhui ya ngano yameathirika kutokana na mabadiliko ya kiteknolojia, hivyo kupunguza uhalisia wa simulizi za kitamaduni. Utafiti unahitimisha kuwa sayansi na teknolojia zimechangia uhifadhi wa ngano, lakini matumizi yasiyozingatia maadili ya jadi yanaweza kuhatarisha urithi wa ngano za Kisukuma. Inapendekezwa kuwa matumizi endelevu ya teknolojia yafanyike kwa kulinda na kudumisha ngano za Kisukuma kwa vizazi vijavyo

Upakuaji

Bado hatuna takwimu za upakuaji.

Marejeleo

Allahyari, T., Rangi, N. H., Khosravi, Y., & Zayeri, F. (2011). Development and evaluation of a new questionnaire for rating of cognitive failures at work. International Journal of Occupational Hygiene, 3(1), 6-11.

Azizi, A. (2014). Athari za Maendeleo ya Sayansi na Teknolojia Kwenye Nyimbo za Asili za Wapare (Master's thesis, University of Dodoma (Tanzania)).

Campbell, S., Greenwood, M., Prior, S., Shearer, T., Walkem, K., Young, S., Bywaters, D., & Walker, K. (2020). Purposive sampling: complex or simple? Research case examples. Journal of Research in Nursing, 25(8), 652–661.

Elfil, M., & Negida, A. (2019). Sampling methods in clinical research; an educational review. Archives of Academic Emergency Medicine, 7(1), 3–5.

Faustine, S. (2020). Msukumo wa jamii katika mabadiliko ya utendaji wa tamthilia ya kiswahili. Mulika Journal.

Florence, A. M., & Lihanda, M. K. (2024). Teknolojia ibuka na ufundishaji wa somo la Kiswahili. Eastern Africa Journal of Kiswahili, 3(1), 25-32.

Forero, R., Nahidi, S., De Costa, J., Mohsin, M., Fitzgerald, G., Gibson, N., McCarthy, S., & Aboagye-Sarfo, P. (2018). Application of four-dimension criteria to assess the rigour of qualitative research in emergency medicine. BMC Health Services Research, 18(1), 1–11.

Gwet, K. L. (2012). Handbook of inter-rater reliability: The definitive guide to measuring the extent of agreement among multiple raters MD. Advanced Analytics Press.

Juma, S. K. (2011) “Athari chanya na hasi za maendeleo ya sayansi na teknolojia katika fasihi Simulizi,” Tasinifu ya shahada ya umahiri ya Kiswahili ya Chuo Kikuu Cha Dodoma.

Kaishozi, J. F. (2021) “Maendeleo ya sayansi na teknolojia na uhai wa michezo ya watoto,” Tasinifu ya shahada ya Umahiri ya Kiswahili ya Chuo Kikuu Huria cha Tanzania.

Kasiga, G. A., & Luhwago, N. J. (2020). Filamu ya Kiswahili: Fasihi Simulizi Iliyostawi. Mwanga wa Lugha, 5(1), 107-124.

Kasiga, G. A. (2022). Miktadha ya Matumizi ya U-Nigeria katika Video za Nyimbo za Muziki wa Kizazi Kipya Nchini Tanzania. Nuru ya Kiswahili, 1(2), 184-211.

Kasiga, G. A. (2023). Tathmini ya Nyimbo za Muziki wa Kizazi Kipya Karne ya 21 Nchini Tanzania: Tija na Madhara yake. Mulika Journal, 42(1), 66-82.

Kassim, B. O., Mraiji, J. K., & Manasseh, L. (2020). Aina ya Nyenzo Katika Ufundishaji wa Fasihi Simulizi ya Kiswahili Katika Shule za Sekondari Nchini Kenya. Jarida la Afrika Mashariki la Masomo ya Kiswahili, 2(2), 143-152.

Khalili, O. E. (2018). Uimarishwaji Wa Umaizi Mseto Kupitia Mikakati Shirikishi Ya Ufundishaji Wa Kiswahili Nchini Kenya.

Lukamika, K. M. (2022). Je, Kuna Matapo katika Fasihi Simulizi? Jarida la Afrika Mashariki la Masomo ya Kiswahili, 5(2), 58-68

Mbarouk, M. J. (2015). Athari za sayansi na teknolojia katika hadithi za watoto: mifano ya ngano kutoka wilaya ya Micheweni Pemba (Doctoral dissertation, Chuo Kikuu cha Dodoma).

Mdee, J. S na Mrikaria, G (2006) Nadharia ya Fasihi Simulizi na Maendeleo katika Sayansi Teknolojia katika Mulika Juzuu 27, Taasisi ya Uchunguzi wa Kiswahili, Dae es salaam.

Mdowe, S. R. (2011) “Nyimbo za michezo ya watoto zinavyobadilika na wakati kifani na kimaudhui katika wilaya ya Magharibi Unguja,” Tasinifu ya shahada ya Umahiri ya Kiswahili ya Chuo Kikuu cha Dodoma.

Mrikaria, S. E. (2007) “Fasihi simulizi na teknolojia mpya,” katika Swahili Forum 14:197-206.

Mtega, W. S. (2021). Ufasihi wa Matambiko: Uchunguzi wa Matambiko ya Wapangwa. Kioo cha Lugha.

Mulokozi, M. M. (1996) Fasihi ya Kiswahili. Dar es Salaam: Chuo Kikuu Huria cha Tanzania.

Munyengabire, S. (2024). TEHAMA na Athari zake katika Ufundishaji na Ujifunzaji wa Kiswahili katika Shule Teule za Sekondari Nchini Rwanda. Jarida la Afrika Mashariki la Masomo ya Kiswahili, 7(1), 155-169.

Mutembei, A (2005) Uwasilishwaji, Uhufadhi na Usambazaji Fasihi Simulizi hapo Kale na Sasa katika Mulika Vol 27: 11 TUKI.

Mutembei, A. K. (2006) “Nadharia ya fasihi simulizi na maendeleo katika sayansi na teknolojia,” katika Mulika 27:1-17.

Robin, B. R. (2016) “The power of digital storytelling to support teaching and learning,” in Digital education review 30: 17-29.

Salim, M. A. (2015). Kuchunguza Ufasihi Simulizi unaojitokeza Ndani ya Hadithi za Kusadikika na Adili na Nduguze (Doctoral dissertation, The Open University Of Tanzania).

Sanga, A. N. (2021). Thamani ya Ujumi wa Kiafrika katika Hadithi Fupi Simulizi za Kiswahili. Mulika Journal.

Senkoro, F. E. M. K. (2011). Fasihi. Dar es Salaam: Dar es Salaam University Press.

Simiyu, W. F. (2011) Kitovu cha Fasihi Simulizi. Mwanza: Serengeti Book Shop.

Songoyi, E. M (1997). OLT 103 1: Oral Literature 1. Daressalaam, Open University of Tanzania.

Sululu, S. B., Wafula, R. M., & Maitaria, J. N. (2021). Mchango wa Tanzu za Kimaigizo za Fasihi Simulizi Katika Umahuluti wa Riwaya ya Kiswahili: Uchunguzi wa Riwaya ya Kufa Kuzikana. Jarida la Afrika Mashariki la Masomo ya Kiswahili, 3(1), 91-99.

Stephano, R. (2020). Utoshelevu wa Mawasiliano kwa Kiswahili katika Teknolojia ya SIKANU:: Uchunguzi Kifani wa WhatsApp. JULACE: Journal of the University of Namibia Language Centre, 5(1), 1-14.

Taherdoost, H. (2018). Sampling Methods in Research Methodology; How to Choose a Sampling Technique for Research. SSRN Electronic Journal, 5(2), 18–27.

Wamitila, K. W. (2003). Kichocheo cha Fasihi Simulizi na Fasihi Andishi. Nairobi: Focus Publications Ltd.

Wanjala, S. F. (2020). Safina ya Utafiti wa Fasihi Simulizi. Kakamega: Elgon Epitome Publishers Ltd.

Yamac, A. & Ulusoy, M. (2017) “The effect of digital story telling in improving the third grader’s writing skills,” International electronic journal of elementary education, 9 (1): 59-86.

Yamane, Taro. (1967). Statistics, An Introductory Analysis, 2nd ed., NewYork: Harper and Row

Tarehe ya Uchapishaji
12 November, 2025
Jinsi ya Kunukuu
Balele, J., & Maguo, M. (2025). Athari za Maendeleo ya Sayansi na Teknolojia Kwenye Ngano za Jamii ya Wasukuma. Jarida La Afrika Mashariki La Masomo Ya Kiswahili, 8(3), 33-49. https://doi.org/10.37284/jammk.8.3.3955