Uhakiki wa Mandhari katika Riwaya Teule za Kiswahili: Tumaini na Kala Tufaha
Ikisiri
Mandhari ni kipengele muhimu katika kufanikisha maudhui ya mwandishi. Kwa kawaida mandhari hushirikiana na vipengele vingine vya fani ili kufaulisha uwasilishaji wa maudhui yanayokusudiwa na msomaji. Utukiaji wa maswala katika jamii hufanyika katika sehemu mahususi yaani mandhari, vivyo hivyo kazi za kifasihi nazo hufuata mkondo uo huo kwa sababu fasihi hupata malighafi yake katika mazingira ya mtunzi. Mtunzi wa kazi ya fasihi ana uwezo wa kutumia mandhari halisi au mandhari ya kufikirika katika mchakato mzima wa kuwasilisha maudhui yake. Utafiti huu hivyo basi, ulilenga kuchunguza jinsi mandhari yanavyotumika kukuza maudhui katika riwaya ya Clara Momanyi Tumaini (2006) na Babu Omar Kala Tufaha (2007). Ili kutimiza lengo hili, Nadharia ya Uhalisia ilitumika.Nadharia hii iliasisiwa na Hegel. Waitifaki wa Nadharia hii ni George Lukas (1972) na wengine.Utafiti huu ulikuwa wa kimaelezo na ulifanyika katika maktaba. Sampuli ilichaguliwa kwa njia ya kimakusudi kwa kulenga riwaya maalum. Baadaye data ilichanganuliwa kwa njia ya kimaelezo kwa mujibu wa mihimili ya Nadharia ya Uhalisia pamoja na lengo la utafiti huu ambalo ni; kutathmini mchango wa mandhari katika kukuza maudhui katika riwaya teule
Upakuaji
Marejeleo
Donna, E.N. (1992). The Impact of Literature Based Reading.Upper Saddle: Pearsom Education.
Kanyua, G.M. (2013). “Mtindo Unavyoendeleza Maudhui katika Natala”. Tasnifu ya Uzamili, Chuo Kikuu Cha Nairobi. (Haijachapishwa)
Kang`eri, S.N. (2017). Uchunguzi wa Vipengele Teule vya Fani katika Riwaya ya Mashetani wa Alepo”. Tasnifu ya Uzamili, Chuo Kikuu cha Nairobi. (Haijachapishwa)
Lukacs, G. (1972). Studies In European Realism: A Sociological Survey Of Writings Of Balzac, Stendhal, Zola, Tolstoy Gorki &Others. London: Marlin Press.
Millet, K.(1069).Sexual Politics.New York: Doubleday and Company Inc.
Momanyi, C. (1998). “Usawiri wa Mwanamke Katika Jamii ya Waswahili Kama Inavyobainika Katika Ushairi wa Kiswahili.” Tasnifu ya Uzamifu: Chuo Kikuu cha Kenyatta. Haijachapishwa.
_____________ (2006). Tumaini.Nairobi: Video-Muwa Publishers.
Mbuthia, E.M. (2005). “A Stylistic and Thematic Analysis of Kiswahili Short Stories”. Tasnifu ya Uzamifu, Chuo Kikuu cha Nairobi. (Haijachapishwa).
Njogu, K. na Chimerah, R. (1999). Ufundishaji wa Fasihi: Nadharia na Mbinu.Nairobi. Jomo Kenyatta Foundation.
Ndungo, C.M.(1985).`Wanawake na Mabadiliko ya Kihistoria katika fasihi ya Kiswahili`.Tasnifu ya Uzamili,Chuo Kikuu cha Nairobi.
Omar, B. (2009). Kala Tufaha.Nairobi: Oxford Publishers Ltd.
Wamitila, K. W. (2002). Uhakiki wa Fasihi; Nadharia na Mbinu. Nairobi: Phoenix Publishers.
Copyright (c) 2025 John Kariuki, Kawira Kamwara

This work is licensed under a Creative Commons Attribution 4.0 International License.